
Makumi ya watu wameuawa hadi sasa tangu
kuanza tena mapigano katika mkoa wa Tanganyika nchini Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo mwezi Julai mwaka jana.
Richard Ngoie Kiatngala, Gavana wa mkoa wa Tanganyika mashariki
mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesisitiza wakati wa kuanza
kikao cha kujadili amani na suluhu kati ya makabila ya Luba (Bantu) na
Pygmees kuwa, katika mapigano hayo watu 150 wameuawa hadi sasa, 200
wamejeruhiwa, shule 400 zimebomolewa na vijiji 422 kuchomwa moto. Gavana
huyo wa mkoa wa Tanganyika ameongeza kuwa kesi 200 za ubakaji
zimethibitishwa kutokea kufuatia mapigano hayo ya kikabila; huku
asilimia 76.4 ya wakazi wa mkoa wa Tanganyika wakikabiliwa na uhaba wa
chakula na mlipuko wa maradhi ya kipindupindu na surua.

No comments:
Post a Comment