Thursday, August 31, 2017

MAWAZIRI WA NJE WA UJERUMANI NA MAREKANI WAKUBALIANA

Ujerumani na Ulaya zinataka kuhakikisha vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Urusi havisababishi kuzuka kwa enzi mpya ya uhusiano mbaya kati ya Urusi na nchi za Magharibi

USA Gabriel bei Tillerson in Washington (picture-alliance/AP-Photo/S. Serkan Gurbuz)
Hayo yameelezwa na waziri wa mambo ya nchi za nje wa  Ujerumani Sigmar Gabriel baada ya mazungumzo  na Waziri mwenzake wa Marekani Rex Tillerson mjini washington.
Waziri Gabriel alisema alizungumza na  na Tillerson jana na kuongeza kwamba  amefurahishwa  kwamba Rais Donal Trump wa Marekani amekubali kuwa na ushirikiano na washirika  wa Marekani kuhusu hatua  zaidi za baadaye. Gabriel alisema , " sisi kama Waulaya tuna wasiwasi mkubwa kwamba  hili litakuwa na athari isiyotarajiwa kwa Ulaya. Hatutaki kuharibu kabisa  uhusiano wa kibiashara na  Urusi hasa katika sekta ya nishati."
Mnamo mwezi huu Rais Trump  aliidhinisha vikwazo vipya dhidi ya Urusi kutokana na hatua yake ya kulitwaa jimbo la  ukraine la Crimea  2014, na  kwa kile kilichoelezwa na  duru za usalama  za Marekani kuwa ni kujiingiza kwa Urusi katika mchakato wa uchaguzi wa Marekani, dai ambalo Urusi imelikanusha.
Gabriel ameikosoa Marekani kwa kuchukua hatua hiyo na kwamba itasababisha makampuni ya Ujerumani yanayohusika na miradi ya nishati nchini Urusi kutozwa faini kwa kukiuka sheria ya  Marekani na kusababisha enzi ya mvutano mpya kati ya  Urusi na Marekani na pia  na nchi nyengine za magharibi.
Brigitte Zypries Bundeswirtschaftsministerin SPD (picture-alliance/dpa/S. Pförtner)
Waziri wa uchumi wa Ujerumani Brigitte Zypries
Kwa upande mwengine waziri wa  uchumi wa Ujerumani Brigitte Zypries ameutaka Umoja wa Ulaya  ulipize kisasi dhidi ya  Marekani ikiwa vikwazo vipya dhidi ya Urusi vitapelekea makampuni ya Ujerumani kuadhibiwa.
Mwakilishi  mpya mteule wa Marekani nchini Ukraine Kurt Volker aliiambia Deutsche Welle kwamba Marekani haitokuwa na mkataba mwengine na  Urusi bila ya kuzingatia ridhaa ya ukraine au  kushauriana na  Ulaya. Alisema  Marekani imeeleza wazi inaunga mkono kikamilifu mchakato wa Normandy na haina  nia ya kuwa sehemu ya utaratibu huo au kukiuka yaliofikiwa. 
Mapema wiki hii, Kansela Angela Merkel wa Ujerumani na rais Emmanuel Macron wa Ufaransa walitowa wito kuwataka wanajeshi wa Ukraine na wapiganaji wanaotaka kujitenga  wakiungwa mkono na Urusi, kuzidisha juhudi ili kuyatekeleza makubaliano ya usimamishaji mapigano.  Mzozo huo umeshasababisha kupotea kwa  maisha ya zaidi ya watu 10,000. Merkel aliwaambia  waandishi habari jana  kwamba vikwazo dhidi ya Urusi vitaondolewa pale hali  itakapoboreka, mashariki mwa Ukraine.
Gabriel leo yuko mjini Paris  alikoelekea moja kwa moja baada ya ziara yake mjini Washington.  Amekutana na  Rais Emmanuel Macron na amepangiwa pia kuhudhurai kikao cha baraza la mawaziri baada ya mazungumzo yake katika ikulu ya Elysee.
Mwandishi: Mohammed Abdul-Rahman, Reuters, dpa
Mhariri:Iddi Ssessanga

TRUMP AKATAA SULUHUHISHO LA KIDIPLOMASIA KOREA KASKAZINI

Rais wa Marekani, Donald Trump na waziri wake wa ulinzi wametoa kauli zinazotofautiana kuhusu Korea Kaskazini, huku Trump akisema mazungumzo sio jibu la kuondoa wasiwasi uliopo wa makombora yanayorushwa na nchi hiyo.

KUSHTADI MAUAJI YANAYOFANYWA NA SAUDIA DHIDI YA WATOTO WA YEMEN NA WASIWASI WA JAMII YA KIMATAIFA

Kanali ya televisheni ya Al Mayadeen ya Lebanon imetangaza kuwa watoto wa Yemen wamegeuzwa dango za kutungia shabaha makombora ya ndege za kivita za Saudi Arabia; na hadi sasa karibu watoto elfu tatu wamepoteza maisha katika mashambulio ya anga yaliyofanywa na ndege hizo.
Al- Mayadeen imeongeza kuwa mashambulizi hayo yamejeruhi pia watoto 2,400 na hii ni katika hali ambayo jamii ya kimataifa imeendelea kunyamazia kimya jinai zinazofanywa na Saudia nchini Yemen.
Utawala wa Aal Saud ulianzisha mashambulio ya kijeshi dhidi ya Yemen tangu mwezi Machi 2015 kwa uungaji mkono wa Marekani na baadhi ya nchi za Kiarabu za eneo hili. Mashambulio hayo hadi sasa yameshaua zaidi ya Wayemeni 12,000 na kuwajeruhi maelfu ya wengine, wengi wao wakiwa ni watoto wadogo. 
Kutokana na hali hiyo shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch pamoja na mashirika mengine 56 yasiyo ya kiserikali yamelitaka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa liunde jopo huru la kuchunguza vitendo mbalimbali visivyo vya kiutu, ukiukaji wa sheria za kimataifa za haki za binadamu na wa sheria za masuala ya kibinadamu uliofanywa nchini Yemen. Ulegevu unaoendelea kuonyeshwa na jamii ya kimataifa mbele ya utawala unaoua watoto wasio na hatia wa Yemen umeupa jeuri utawala huo wa Aal Saud ya kushadidisha jinai zake ikiwemo ya kuua raia zaidi wa Yemen. Kwa kufanya mauaji ya watoto wadogo, Saudi Arabia unataka kuzusha hali ya woga na hofu ili kuwafanya wananchi wa Yemen wasalimu amri mbele ya malengo yake ya kujipanua.
Kuhusiana na suala hilo, gazeti linalochapishwa Dublin, Ireland la Irish Timeslimeashiria taarifa ya pamoja ya wakurugenzi wa taasisi tatu zilizo chini ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali mbaya ya kibinadamu inayotawala nchini Yemen, na kuandika: 
"Vita vya Yemen-Vita dhidi ya watoto".
Wachambuzi wa siasa wameyaelezea mauaji ya halaiki kama ya wananchi wa Yemen yanayofanywa na Saudia kuwa ni moja ya aina mbaya zaidi za ugaidi.
Katika hali na mazingira kama hayo, misimamo ya Katibu Mkuu wa sasa na aliyetangulia wa Umoja wa Mataifa imekuwa ikikosolewa vikali kutokana na kutamka dhahiri shahiri au kwa namna isiyo ya wazi kwamba haiwezekani kulaani mauaji ya watoto wa Yemen kutokana na utegemezi ulionao umoja huo kwa Saudia. Misimamo hiyo inadhihirisha hali mbaya na ya kusikitisha ya kiakhlaqi na kiutu waliyonayo wanasiasa na shakhsia muhimu wa kimataifa. Hatua ya Ban Ki-Moon, Katibu Mkuu aliyetangulia wa Umoja wa Mataifa ya kuiondoa Saudi Arabia kwenye orodha nyeusi ya nchi zinazokiuka haki za watoto na uzembeaji uliofanywa na Katibu Mkuu wa sasa Antonio Guterres wa kushindwa kurekebisha utendaji mbovu wa mtangulizi wake katika kadhia hiyo na kuendelea kuonyesha ulegevu mbele ya jinai zinazofanywa na Saudia vimechangia sana kuufanya utawala huo wa kifalme uwe na jeuri ya kuendeleza jinai zake nchini Yemen.
Baada ya kushindwa kufikia malengo yake nchini Yemen, utawala wa Aal Saud umeshadidisha jinai zake nchini humo kwa kiwango cha kutisha zaidi ili kujaribu kufifilisha kushindwa kwake huko. Hali hiyo imewafanya walimwengu waendelee kushuhudia kila leo maafa yanayowasibu wananchi wa Yemen kutokana na jinai za utawala wa Saudi Arabia dhidi ya wananchi hao wasio na mlinzi.
Profesa Rodney Shakespeare, mchambuzi wa masuala ya kisiasa wa Uingereza anaizungumzia nukta hiyo kwamba:
"Uvamizi uliofanywa na Saudi Arabia dhidi ya Yemen na mauaji ya wanawake na watoto wa nchi hiyo ni jinai ya mauaji ya kimbari".
Kwa kuua hata watoto wadogo, Saudia ambayo ni nembo ya Uwahabi na muenezaji itikadi potofu za kitakfiri na kisalafi imeonyesha kuwa haina mpaka wowote iliojiwekea katika kufanya jinai; na ni kwa kushadidisha jinai hizo tu ndipo itaweza kutuliza kiu yake ya ukatili na umwagaji damu. Mwenendo wa aina hii unakumbusha jinai na ukatili wa Unazi, Ufashisti na Uzayuni katika uga wa uhusiano wa kimataifa.../

WAROHINGYA 17 WAFARIKI KATIKA MPAKA WA MYANMAR NA BANGLADESH

Kwa askali wakimbizi 17 Waislamu wa kabila la Rohingya wamekufa maji katika mpaka wa Myanmar na Bangladesh wakikimbia jinai wanazofanyiwa na Mabudha wenye misimamo ya kuchupa mipaka na jeshi la Myanmar.
Gadi ya Pwani ya Bangladesh mapema leo Alkhamisi imegundua miili 17 ya wakimbizi hao, aghalabu ya maiti hizo zikiwa ni za watoto wadogo, katika ufukwe wa Mto Naf, ulioko katika mpaka wa Myanmar na Bangladesh.
Miili hiyo ya wakimbizi Waislamu wa Rohingya imepatikana siku moja baada ya miili mingine miwili ya wanawake na miwili ya watoto kupatikana katika ukingo wa mto huo.
Tangu Ijumaa iliyopita, jeshi la Myanmar limewaua Waislamu zaidi ya 100 katika jimbo la Rakhine katika wimbi jipya la mauaji dhidi ya Waislamu nchini Myanmar. Mauaji hayo yamepelekea maelfu ya Waislamu kukimbilia Bangladesh wakihofia hujuma zaidi za jeshi na Mabudha wenye misimamo mikali.
Waislamu wakimbizi wa Rohingya katika eneo la mpakani na Bangladesh
Mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanywa na Mabudha wenye misimamo mikali na wanajeshi wa Myanmar dhidi ya Waislamu wa Rohingya katika mkoa wa Rakhine magharibi mwa nchi hiyo tangu miaka kadhaa iliyopita hadi sasa yamesababisha kuuliwa na kujeruhiwa maelfu ya Waislamu hao na kuwafanya makumi ya maelfu ya wengine kuwa wakimbizi. 
Kuna Waislamu zaidi ya milioni moja na laki tatu nchini Myanmar lakini serikali ya nchi hiyo imekataa kuwapa haki zao za kimsingi hasa uraia.

Sunday, August 27, 2017

UN: MSAADA WA CHAKULA UNAHITAJIKA KWA AJILI YA WAKIMBIZI NCHINI TANZANIA

Mpango wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (WFP) umesema umepunguza mgawo wa chakula kwa wakimbizi 320,000 wanaoishi kaskazini magharibi mwa Tanzania kutokana na kupungua misaada ya kifedha.
WFP imesema katika taarifa yake leo kuwa inahitaji haraka fedha kiasi cha dola milioni 23.6 ili kukidhi mahitaji ya chakula kwa wakimbizi hadi kufikia mwezi Disemba. Wakimbizi walioathiriwa na upungufu wa chakula ni kutoka Burundi na Kongo.
Wakimbizi kutoka Burundi na Kongo waishio Tanzania  
Michael Dunford Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania amesema kuwa punguzo jingine la mgawo wa chakula litatekelezwa iwapo wafadhili hawataitikia haraka maombi ya kuchangia misaada ya kifedha.  Umoja wa Mataifa pia umekuwa ukiitilia mkazo jamii ya kimataifa kutoa mchango ili kuwasaidia wakimbizi wa Sudan Kusini zaidi ya milioni mbili waliopata hifadhi katika nchi jirani. 

USAFIRISHAJI BIDHAA ZA IRAN NCHINI KENYA KUONGEZEKA KWA ASILIMIA 100 KATIKA MWAKA 2017

Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Kenya amesema usafirishaji bidhaa zisizo za mafuta za Iran kuelekea nchini Kenya katika miezi sita ya kwanza ya mwaka huu wa 2017 ulikuwa wa kiwango cha dola milioni 58 na inakadiriwa kuwa hadi ifikapo mwishoni mwa mwaka huu kiwango hicho kitaongezeka kwa kasi kubwa na kufikia asilimia 100.
Hadi Farajvand ameyasema hayo leo kuhusiana na hatua zilizochukuliwa na ubalozi wa Iran mjini Nairobi kwa ajili ya kustawisha uhusiano wa kibiashara na Kenya na kuongeza kuwa: Mashirika ya Kiirani yanayoshughulika sekta za biashara, uchumi na utoaji huduma na kiufundi na kiuhandisi yamepata fursa nzuri za kutangaza bidhaa na huduma zao katika soko la Kenya na pia kwenye masoko ya nchi nyingine za Afrika Mashariki.
Hadi Farajvand, Balozi wa Iran nchini Kenya
Farajvand amebainisha kuwa, katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mashirika ya Kiirani yamekamilisha miradi ya utoaji huduma za kiufundi na kiuhandisi yenye thamani ya zaidi ya dola milioni mia moja na hivi sasa yanaendelea na mazungumzo kwa ajili ya kufunga mikataba mingine ya miradi ya ujenzi wa mabwawa, vinu vya umeme wa nishati ya maji na mabomba ya usafirishaji fueli.
Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Kenya ameeleza kwamba kuandaa ratiba kwa ajili ya safari ya jumbe za kiuchumi za Kenya nchini Iran na kuandaa maonyesho ya kwanza maalumu ya Iran mjini Nairobi ni miongoni mwa hatua zinazochukuliwa na ubalozi wa Iran mjini Nairobi kwa lengo la kuongeza kiwango cha usafirishaji bidhaa za Iran na utoaji huduma za kiufundi na kiuhandisi nchini Kenya.../

MBUNGE WA JIMBO LA MKURANGA MGENI RASMI KATIKA MAHAFALI DARASA LA SABA


 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Mkokozi, Makariusy Kihawa akizungumza jambo wakati wa Mahafali ya Nne yaliyofanyika Mkuranga, Mkoa wa Pwani,   jana. ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Abdallah Ulega (pichani hayupo) (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega (wapili kulia) akisaini katika kitabu cha wageni, wa kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Shule, Bakari Mtulia na kulia ni Diwani wa Kata ya Mwandege Wilaya ya Mkuranga, Adolph Koelo
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega (aliye simama) akizungumza jambo na katika  mahafali ya Darasa la Saba 
Baadhi ya wanafunzi wakionyesha jinsi juice na chama (chipsy) zinavyo changia kuongeza maradhi
Baadhi ya wanafunzi wakionyesha wazazi mambo waliyofundishwa Shule hapo ambayo ni ya Kisayansi zaidi, nakuwaasa wazazi wao kuacha kuwanunulia juice na chipsy (chama)

Moja wa wanafunzi akionyesha jinsi chama inayo kuwa kama gundi na akahoji, anatumia maji kukosha na haitoki je, tumboni utakosha na nini
Mwanafunzi, Ally Chizoro akionyesha paketi ya chipsy na akatoa wito kwa wazazi kutopenda kuwanunulia kitu hicho kwani vina madhara

Mwalimu wa Sayansi na Hisabati Shule ya Msingi Mkokozi, Anthony Ungelleh akisisitizia jambo hilo la kutopenda wazazi kuwanunuli chama watotowao na juice 
Mwanafunzi, Ally Chizoro akigawa chama (chipsy) na akatoa wito kwa wazazi kutopenda kuwanunulia kitu hicho 
Wazazi 
Wazazi wakifatilia Mahafali hayo kwa umakini mkubwa
Wanafunzi wanao hitimu Darasa la Saba wakicheza kwaito
Walimu wakishirikiana na wanafunzi wanao hitimu kucheza kwaito
Mwalimu Aneth Msuya akitoa burudani pamoja na wahitimu hao wakati wa Mahafali yao jana
Mbunge wa jimbo hilo akiwasili viwanja vya Shule hiyo
Mwalimu wa Taaluma,  Hadija Maarifa (kushoto)  akiwaongoza wahitimu hao kuimba nyimbo 
Afisa Elimu Kata ya Mwandege, Zainabu Mangare (kushoto) akimkabidhi mhitimu Bilali Mussa wakati wa mahafali hayo baada ya Mbunge kufungua 
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega (wa pili kushoto) akimkabidhi cheti Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mkokozi, Ally Chizora  aliyeshika nafasi ya kwanza kati ya wanafunzi 139  darasani, Kata na Wilaya wakati wa Mahafali ya Nne yaliyofanyika, Mkuranga, Mkoa wa Pwani jana.





GALLUP: WAMAREKANI WEUSI ZAIDI 220 WAMEUAWA NA POLISI YA NCHI HIYO MWAKA ULIOPITA

Zaidi ya Wamarekani 220 wenye asili ya Afrika wameuawa kwa kupigwa risasi na polisi ya nchi hiyo katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Gazeti la Kimarekani la Huffington Post limetoa ripoti ya mwaka mmoja baada ya mchezaji wa futboli wa Marekani, Colin Kaepernick kulalamika dhidi ya ubaguzi wa rangi na mauaji yanayofanywa na polisi ya nchi hiyo dhidi ya Wamarekani weusi na kuandika kuwa: Katika kipindi hicho cha mwaka mmoja wanamichezo waliopinga ubaguzi wamebakia hivi hivi bila ya ajira, na polisi imeua raia wengine weusi wasiopungua 223.
Huffington Post limeandika kuwa, kuwa uwezekano kwamba idadi ya Wamarekani weusi waliouawa na polisi ya nchi hiyo ni kubwa zaidi na kuongoza kuwa: Katika kesi 160 za mauaji hayo yaliyofanywa na polisi katika kipindi cha tarehe 14 Agosti 2016 hadi 14 Agosti 2017 mbari ya wahanga hao haikutajwa au kuthibitishwa. 
Wamarekani wakimuunga mkono Colin Kaepernick 
Sambamba na mauaji ya Wamarekani weusi, malalamiko ya kupinga ubaguzi nchini Marekani bado yanaendelea na wachezaji wengi wa soka wa lipi ya NFL wamejiunga na Colin Kaepernick. Gazeti la Kimarekani la Huffington Post limeongeoza kuwa: Wamarekani wengi weusi waliouawa kwa kupigwa risasi na polisi hawakuwa na silaha. 
Wakati huo huo matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi ya Forward Institute yanaonesha kuwa, thuluthi mbili ya vijana wa Marekani wenye asili ya Afrika na karibu nusu ya Malatino wamekumbana na maudhi na ukatili wa polisi ya nchi hiyo. 

NASAHA ZA KIONGIOZI MUADHAMAMU WA MAPINDUZI YA KIISLAMU KWA SERIKALI YA RAIS ROUHANI

Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu jana Jumamosi alionana na Rais Hassan Rouhani na baraza lake la mawaziri kwa mnasaba wa Wiki ya Serikali nchini Iran na kwa mara nyingine amesema kuwa, suala la uchumi ndicho kipaumbele kikuu cha Iran hivi sasa.
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu udharura wa serikali ya Iran kuyapa umuhimu mkubwa masuala ya kiuchumi, ni jambo linalowezi kutathminiwa katika nyuga kadhaa. Moja ya nukta hizo ni uhakika kwamba uchumi dhaifu una madhara mengi sana na ya muda mrefu. Nchi huru duniani haipaswi kuruhusu bei za bidhaa kupanda ovyo, au kuzorota uchumi wake, au kuweko juu kiwango cha ukosefu wa kazi au jamii ya nchi hiyo kukumbwa na ugonjwa wa kupenda kutumia bidhaa za kigeni na kudharau bidhaa zao wenyewe. Moja ya sababu ya kuweko jambo hilo inaweza kuwa ni vikwazo na mashinikizo ya kigeni, lakini chanzo chake kikuu ni kutegemea pato la mafuta na wakati bei ya mafuta inapoporoka katika soko la dunia, uchumi wa nchi hupata pigo kubwa. Ni kwa kutilia mkazo suala hilo ndio maana Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu akasema kuwa, kuna wajibu kwa uchumi wa Iran kuacha kabisa kutegemea pato linalotokana na kuuza nje mafuta ghafi.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika mazungumzo na Rais Rouhani na baraza lake la mawaziri

Jambo hilo linaweza kufanikishwa kwa kuzingatia suhula, uwezo wa kila namna na nguvu kazi mahiri iliyopo nchini Iran; lakini pia lina masharti yake. Kuliko wakati mwingine wowote, hivi sasa Serikali ya Iran ina jukumu kubwa zaidi la kuwa na mipangilio mizuri na kutumia ipoasavyo suhula na nguvu kazi iliyopo nchini katika jitihada za kukuza uchumi na kutoruhusu kabisa suala hilo kuathiriwa na masuala mengine. Takwimu mbalimbali zinaonesha kuweko mafanikio katika juhudi hizo lakini bado kuna safari ndefu ya kufikia kwenye ustawi wa kiuchumi unaokusudiwa na Jamhuri ya Kiislamu.
Kuchukuliwa hatua kama kuimarisha uzalishaji wa bidhaa za ndani, kuuza huduma za teknolojia na kutegemea elimu za kimsingi katika sehemu muhimu na nyeti za kiuchumi hususan kupambana vilivyo na ufisadi na magendo nchini ni katika mambo ambayo yamekuwa yakisisitiziwa mno na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Katika maadhimisho ya Wiki ya Serikali, Rais Rouhani na baraza lake la mawaziri wakisoma Qurán katika Haram ya Imam Khomeini MA, mwasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kusini mwa Tehran

Kama alivyoashiria katika hotuba yake ya jana, maafisa wa Iran wanapaswa kufanya kazi kimapinduzi katika siasa za nje na kwenye upeo wa kidiplomasia. Amesema, kulindwa msimamo na muelekeo wa kimapinduzi na kidini katika siasa za kigeni za Iran ni jambo muhimu sana. Kama ambavyo amesema pia kuwa, inabidi katika uwanja wa udiplomasia kuwe na uharakishaji mambo, kwenda na wakati na watu kuwa macho na kusisitiza kuwa, watu walioko katika masuala ya kidiplomasia humu nchini wana wajibu wa kuona fakhari kuwa ni wanamapinduzi na wajivunie kusimama imara katika ufanikishaji wa malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu kama vile kusimama kidete kukabiliana na uistikbari, kupiga vita dhulma na kupinga mfumo wa kibeberu.
Kwa kweli ni jambo lisilo na shaka kwamba maadui wa taifa la Iran wataendelea kufanya njama za kila namna za kuikwamisha Jamhuri ya Kiislamu kufikia malengo yake hasa ya kiuchumi.
Miongozo iliyotolewa jana na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa mnasaba wa kuanza kazi serikali ya 12 ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa hakika imebainisha nukta muhimu sana nayo ni kwamba, kwa kuzingatia changamoto nyingi zilizopo, na kuendelea kuweko vikwazao dhidi ya Iran, Serikali ina wajibu wa kuongeza miundombinu ya kiuchumi ili kuandaa mazingira mazuri ya kudumu ya kufanikisha uchumi wa kimuqawama wa kutegemea nguvu za ndani na ambao hautetereshwi na matukio ya nje ya nchi. 

MAULAMAA SUDAN WATAKA KUFUTWA KAZI WAZIRI ANAYETAKA UHUSIANO NA WAZAYUNI

Jopo la Maulamaa wa Sudan limetaka kufutwa kazi waziri wa uwekezaji wa nchi hiyo kutokana na kutoa mwito wa kuweko uhusiano wa kawaida kati ya Sudan na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Muhammed Othman Saleh, Mkuu wa Jopo la Maulamaa wa Sudan amejibu mwito huo wa Mubarak al Fadhil, waziri wa uwekezaji wa Sudan aliyetaka Khartoum iwe na uhusiano wa kawaida na Israel kwa kusema, waziri huyo wa serikali ya Rais Omar al Bashir lazima afutwe kazi kwani mwito wake huo unakwenda kinyume kabisa na misingi na sheria za Sudan.
Muhammad Othman Saleh pia amemtaka  Rais Omar al Bashir kumfukuza mara moja al Fadhil katika Baraza lake la Mawaziri.
Rais Omar al Bashir wa Sudan

Naye Muhammad Hasan Tanun, mjumbe wa Jopo la Maulamaa wa Sudan  amemkosoa vikali Mubarak al Fadhil na kumtaka aheshimu msimamo wa serikali ya Khartoum wa kutokuwa na uhusiano kabisa na utawala wa Kizayuni.
Wiki iliyopita, Mubarak al Fadhil, waziri wa uwekezaji wa Sudan alisema katika kipindi kimoja cha televisheni kwamba haoni tatizo lolote kwa nchi yake kuwa na uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Matamshi ya waziri huyo wa serikali ya Rais Omar al Bashir ymelaaniwa na kulalamikiwa mno na vyama vya kisiasa na taasisi za kidini za Sudan.

19 AKIWEMO MWANAHABARI WA US WAUAWA KATIKA MAPIGANO SUDANI KUSINI

Watu 19 akiwemo mwandishi wa habari raia wa Marekani wameuawa katika mapigano mapya baina ya vikosi vya serikali na waasi wanaobeba silaha katika jimbo la Yei, nchini Sudan Kusini.
Santo Domic Chol, msemaji wa jeshi la Sudan Kusini ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa, mapigano hayo ya jana Jumamosi yalianza baada ya kundi hilo la wabeba silaha kujaribu kuvamia kituo cha kijeshi cha Kaya.
Ameongeza kuwa, waasi 15 wameuawa katika makabiliano hayo huku jeshi la nchi hiyo likipoteza askari wake watatu. 
Wanachama wa genge la waasi Sudan Kusini
Msemaji wa jeshi la Sudan Kusini amesema mwandishi huyo wa habari wa Marekani aliyeuawa katika makabiliano hayo ya jana kati ya wanajeshi wa serikali na waasi ametambuliwa kwa jina Christopher Allen, ambaye alikuwa akifanyia kazi mashirika kadhaa ya habari.
Sudan Kusini ilitumbukia katika machafuko na mapigano kati ya askari watiifu kwa Rais Salva Kiir na makamu wake wa zamani Riek Machar tangu mwaka 2013.
Vita vya ndani katika nchi hiyo changa zaidi barani Afrika vimewalazimisha raia karibu milioni tatu kuwa wakimbizi katika nchi jirani na maelfu ya wengine kuuawa. 

Saturday, August 26, 2017

RAIS MADURO AZUNGUMZIA VIKWAZO VYA KIFEDHA VYA MAREKANI

Rais Nicolas Maduro wa Venezuela jana amesema amri ya Rais Donald Trump wa Marekani inayozuia mapatano kuhusu deni jipya la serikali yake au kampuni ya taifa hilo ya mafuta - PDVSA imekusudia kulikusuma taifa hilo lililokumbwa na mgogoro lishindwe kulipa madeni yake na kimsingi inasababisha kufungwa kwa kampuni yake ya kusafisha mafuta Citgo nchini Marekani. Katika hotuba yake iliyooneshwa kupitia televisheni, akiwa katika makazi yake, Rais Maduro aliongeza kusema kuwa tathmini ya awali unaonyesha vikwazo vitazuia mafuta ghafi ya Venezuela kusafirishwa kwenda Marekani.

TRUMP ATANGAZA MAAFA TEXAS KUTOKANA NA KIMBUNGA HARVEY

Rais Donald Trump wa Marekani amesaini amri ya maafa katika eneo la Texas wakati kimbunga Harvey kikiendelea kuathiri maeneo ya Ghuba ya Pwani. Tangazo la Trump ni hatua ya kuongeza jitihada za msaada katika maeneo ambayo yameathiriwa zaidi. Trump ameyandika hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter akiwa Camp David. Kimbunga hicho kimesababisha maelfu ya watu kuyahama makazi yao na kuvuruga mfumo wa usafiri.

KOREA KASKAZINI YAFYATUA MAKOMBORA YA MASAFA MAFUPI

Korea Kaskazini imefyatua baharini makombora kadhaa ya masafa mafupi kuotokea pwani ya mashariki. Maafisa wa Korea Kusini na Marekani wamethibitisha majaribio hayo. Maafisa wa Marekani wamesema makombora hayo yalifeli

Nordkorea Flagge in Pjöngjang (picture-alliance/AP Photo/Wong Maye-E)
Hayo ni wakati washirika hao wawili, Marekani na Korea Kusini wakifanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi ya kila mwaka ambayo Korea Kaskazini inayaelezea kuwa ni matayarisho ya vita.
Kituo cha jeshi la Marekani katika ukanda wa Pasifik kimesema kiligundua makombora matatu ya masafa mafupi, yaliyofyatuliwa ndani ya kipindi cha dakika 20. Makombora yote matatu yalifeli, ambapo moja lililipuka maramoja baada ya kufyatuliwa, wakati mengine mawili yalishindwa wakati yakiwa angani.
Ofisi ya Korea Kusini ya Wakuu wa Jeshi imesema majaribio hayo yalifanywa kutokea mkoa wa mashariki wa Korea Kaskazini wa Kangwon na yakaruka katika upande wa kaskazini mashariki karibu kilomita 250 kuelekea baharini.
Kamandi ya Pasifik imesema makombora hayo hayakuweka kitisho chochote kwa ardhi ya Marekani wala katika kisiwa chake cha Guam,a mbacho Korea Kaskazini ilitishia mapema mwezi huu kukizingira "katika bahari ya moto”
Kim Jong Un, Donald Trump (picture alliance/AP Photo)
Kim Jong Un na Trump wamepunguza majibizano
Mvutano ulikuwa umepungua tangu majibizano ya maneno makali kati ya Korea Kaskazini na Marekani baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kumuonya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un kuwa angekabiliwa na "moto” kama ataitishia Marekani. Ikulu ya White House imesema Rais Trump amefahamishwa kuhusu makombora hayo lakini hajaweza kutoa kauli yoyote.
Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Marekani haikuzungumzia maramoja kuhusu majaribio hayo ya Jumamosi. Waziri wa Mambo ya Kigeni Rex Tillerson mapema wiki hii aliipongeza Korea Kaskazini kwa kuonyesha kujizuia kwa kutofyatua makombora tangu jaribio la Kombora la Masafa Marefu lililofanywa mwishoni mwa mwezi Julai.
Tillerson alisema anatumai kuwa kutofyatua makombora au kutofanya "vitendo vingine vya uchochezi” kutoka Korea Kaskazini huenda kukaamanisha barabara huenda ikafungua mazungumzo "katika siku za karibuni”.
Trump pia alielezea matumaini mapema wiki hii kuhusu uwezekano wa kuimarika mahusiano. "naheshimu ukweli kwamba anaanza kutuheshimu,” Trump alisema kumhusu Kim.
Vyombo vya habari vya Korea Kaskazini vimeripoti Jumamosi kuwa Kim aliongoza mazoezi ya jeshi la majini na mashambulizi ya angani.

Friday, August 25, 2017

MAFANIKIO MAKUBWA YA MUQAWAMA; KUONGEZEKA KASI YA KUANGAMIZWA KUNDI LA KIGAIDI LA DAESH (ISIS)

Mwenendo wa kuliangamiza na kulitokomeza kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh umezidi kushika kasi kutokana na azma thabiti na mkakati madhubuti unaotekelezwa na mhimili wa muqawama katika mapambano na kundi hilo.
Vikosi vya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh vilivyokuwa vikisindikizwa na magari kadhaa ya deraya na idadi kubwa ya wapiganaji, siku ya Alkhamisi ya tarehe 24 mwezi huu vilijaribu kushambulia kituo kimoja cha jeshi la Syria katika eneo la Saddul-Wa'ar kwenye mpaka wa pamoja wa nchi hiyo na Syria, lakini vilipata kipigo kikali na kurudi nyuma kutoka eneo hilo baada ya wapiganaji wake wengi kuuawa na kujeruhiwa.
Magaidi wa DAESH (ISIS) walipokuwa wamejizatiti Syria
Katika miezi ya karibuni, kundi hilo la kigaidi na kitakfiri limekuwa likishindwa kwa kupata vipigo mtawalia katika maeneo yote liliyokuwa likiyakalia kwa mabavu katika ardhi za Iraq na Syria. Baada ya kukombolewa mji wa Mosul mkoani Nainawa nchini Iraq, magaidi wa kundi la kitakfiri la Daesh wamekuwa wakiendelea kupata vipigo mfululizo katika mji wa Tal afar pia ulioko kwenye mkoa huohuo na hivyo kuzidi kukaribia kusambaratishwa kikamilifu na kutokomezwa katika ardhi ya nchi hiyo. Lakini si huko Iraq pekee; kwani hata nchini Syria pia kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh pamoja na washirika wake wanaendelea kudhoofika na kusambaratika; kiasi kwamba siku chache zilizopita Rais Bashar Al-Assad wa Syria aliashiria kupatikana ushindi kamili katika vita dhidi ya magaidi hao.
Rais Bashar Al-Assad wa Syria akihutubia wananchi
Moja ya sababu muhimu ya kushuhudiwa kasi kubwa ya kusambaratika Daesh na makundi washirika ya kigaidi ni uwezo wa kivita wa mhimili wa muqawama. Hivi sasa vikosi vya kujitolea vya wananchi vimegeuka kuwa nguzo muhimu na imara ya muqawama katika Mashariki ya Kati; mfano hai wa hilo ikiwa ni harakati ya Al-Hashdu-Sha'abi ya Iraq na makundi mengine kadhaa ya wananchi yanayopambana na magaidi wa kitakfiri huko nchini Syria pia. Kuvitumia vikosi vya kujitolea vya wananchi ni moja ya sababu kuu za kuongezeka uwezo wa kivita wa mhimili wa muqawama.
Wapiganaji wa vikosi vya Al-Hashdu-Sha'abi
Lakini kuna nukta nyengine muhimu pia, nayo ni kwamba stratijia ya kila mara ya kivita inayotumiwa na Daesh kwa ajili ya kukabiliana na mkakati wa kivita wa mhimili wa muqawama imeshakuwa butu. Kueneza hofu na vitisho na kutumia ngao ya binadamu katika medani za mapambano ndizo stratijia mbili kuu ambazo zimekuwa zikitumiwa na kundi hilo la kigaidi na kitakfiri. Lakini ujasiri wa vikosi vya mhimili wa muqawama na hamu kubwa ya kufa shahidi waliyonayo wapiganaji wa vikosi hivyo vimeweza kuzima na kuivunja kikamilifu mikakati ya kueneza hofu na vitisho na utumiaji ngao ya binadamu iliyokuwa ikitekelezwa na Daesh. Ni kama alivyosisitiza Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah katika hotuba aliyotoa siku ya Alkhamisi ya kwamba: "Mafanaikio ya operesheni zilizotekelezwa kwenye miinuko ya mpakani mwa Lebanon na Syria, yamepatikana licha ya mbinu na hila zilizotumiwa na Daesh za kuwafanya raia kama ngao ya kibinadamu". Sababu nyengine muhimu iliyowezesha kushindwa mbinu hiyo ya Daesh ni kutumia Hizbullah stratijia ya "mazungumzo sambamba na vita". Mkakati huo umewezesha kuhamishiwa maeneo mengine wapiganaji wa makundi ya kigaidi na kitakfiri. Ni kama lilivyoandika gazeti la Ash-Sharqul-Awsa't kuwa:"Duru za karibu na kundi la kigaidi la Daesh (ISIS) zimetuma mwakilishi wake mmoja kwa viongozi wa Hizbullah ya Lebanon ili kuwafikishia pendekezo la kufikia mapatano. Kwa mujibu wa pendekezo hilo makumi ya wapiganaji wa makundi ya kigaidi wataweza kuhamishiwa eneo la Deir ez-Zor". Kuridhia kufanya mazungumzo kundi la kitakfiri la Daesh maana yake ni kushindwa na kutokuwa na taathira tena mikakati ya kundi hilo ya kueneza hofu na vitisho na kutumia ngao ya binadamu.
Wanamapambano wa Hizbullah, mhimili mkuu wa harakati za muqawama katika Mashariki ya Kati
Nukta ya kumalizia ni kwamba vipigo mtawalia na kushindwa mfululizo Daesh na vikosi vya mhimili wa muqawama kumeitia wasiwasi mkubwa Israel na tab'an baadhi ya nchi za Kiarabu ambazo ni waungaji mkono wa kundi hilo. Kuhusiana na nukta hiyo gazeti la Al-Akhbar limechapa makala iliyoandikwa na Ali Haidar, ambapo mwandishi huyo anasema: "Wasiwasi walionao wapangaji sera na viongozi wa Israel ambao umefichuliwa na kanali ya 10 ya televisheni ya Israel unaendana kikamilifu na msimamo rasmi wa Netanyahu kuhusiana na Daesh. Msimamo ambao Netanyahu ameutangaza rasmi na kuujadili katika mazungumzo na Washington na nchi nyingine za Ulaya na hata akarudia kuusisitizia mara kadhaa ni kwamba 'kuangamizwa Daesh kunamaanisha kushindwa Israel katika vita vinavyofuatia' ".
Kwa maelezo haya tunaweza kusema kuwa kushindwa na kuangamizwa Daesh kutakuwa na matokeo mabaya zaidi kwa Israel kuliko ya kushindwa katika vita vya siku 33 vya mwaka 2006 ilivyoanzisha dhidi ya Hizbullah ya Lebanon.../