Thursday, August 10, 2017

WAANDISHI HABARI WAENDELEA KUKAMATWA UTURUJI

Polisi na vyombo vya sheria wanaendelea kuwaandama  waandishi habari nchini Uturuki. Ripoti kutoka Istanbul zinasema wawakilishi 15 wa vyombo vya habari wamekamatwa. Kwa mujibu wa shirika la habari la serikali, Anadolu, waandishi habari tisa tayari wamekamatwa ikiwa ni pamoja na mhariri mkuu wa gazeti la upinzani " Birgün", Burak Ekici. Waandishi habari waliokamatwa wanatuhumiwa kuwa wanachama wa vuguvugu lililopigwa marufuku la sheikh wa kituruki anaeishi uhamishoni nchini Marekani Fethullah Gülen. Wanatuhumiwa kutumia njia ya mawasiliano-App "Bylook" ambayo hutumiwa zaidi na wafusi wa sheikh huyo wa kidini. Waandishi habari kadhaa wametiwa ndani nchini Uturuki akiwemo pia ripota wa gazeti la "Die Welt" mjerumani mwenye asili ya Uturuki, Deniz Yücel pamoja pia na mkalimani Mesale Tolu.

No comments:

Post a Comment