Tuesday, August 1, 2017

KIONGOZI WA MASHAMBULIZI YA AL-SHABAD AANGAMIZWA SOMALIA

Wizara ya Habari ya Somalia imetangaza kuwa kiongozi wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la ash-Shabab anayehusika na suala la kupanga shambulizi ya kundi hilo ameangamizwa la jeshi la nchi hiyo.
Ali Mohammad Hussein maarufu kwa jina la 'Ali Jabal', alikuwa na jukumu la kuratibu na kutekeleza mashambulizi ya miripuko na mauaji nchini Somalia. Kadhalika Ali Jabal alikuwa akihusika na mashambulizi yaliyowalenga askari wa serikali katika eneo la Toro-toro, kusini mwa nchi hiyo ya pembe ya Afrika.

Wanachama wa genge la ash-Shabab

Hili ni shambulizi la pili la jeshi la Somalia kufanywa katika kipindi cha miezi miwili ya hivi karibuni ambapo idadi kubwa ya vinara wa kundi hilo maarufu kwa kutenda jinai wameuawa. Kundi la kigaidi la ash-Shabab lililazimika kufungasha virago kutoka mjini Mogadishu, mji mkuu wa Somalia mwezi Agosti mwaka 2011 baada ya kushadidi mashambulizi ya jeshi la serikali likishirikiana na askari wa kusimamia amani wa Umoja wa Afrika AMISOM. Hata hivyo genge hilo bado linadhibiti maeneo mbalimbali ya Somalia na linaendelea kufanya hujuma dhidi ya viongozi, askari na raia wa nchi hiyo.

Askari wa Umoja wa Afrika AMISOM

Katika fremu hiyo, Jumatatu ya jana jeshi la Uganda lilitangaza kuwa, askari 12 wa nchi hiyo wameuawa katika shambulizi lililofanywa na wapiganaji wa kundi hilo la kigaidi la al Shabab huko kusini mwa Somalia.

No comments:

Post a Comment