Sunday, October 8, 2017

UN YAYAHADHARISHA HALI YA WAKIMBIZI ELFU 8 WA MYANMAR WALIOPO BANGLADESH

UN yatahadharisha kuhusu hali ya wakimbizi elfu 8 wa Myanmar waliopo Bangladesh
Umoja wa Mataifa umetahadharisha kuwa kutoandaliwa kambi kwa ajili ya kuwahifadhi wakimbizi Waislamu wa Rohingya wapatao elfu nane huko Bangladesh ni jambo hatari sana.
Umoja wa Mataifa umeitahadharisha serikali ya Bangladesh kwa kushindwa kuanzisha nchini humo kambi kwa ajili ya wakimbizi Waislamu wa Rohingya na kuitaka ijenge kambi nyingine ndogo katika maeneo mengine. Serikali ya Bangladesh ilikuwa na mpango wa kujenga kambi ya wakimbizi karibu na mpaka wa Kato Palung kati ya nchi hiyo na Myanmar kufuatia mashinikizo ya jamii ya kimataifa. 
Wakimbizi Waislamu wa Rohingya waliokimbilia Bangladesh  
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kambi za wakimbizi huko Bangladesh hazikuwa katika hali nzuri hata kabla ya kuanza ukandamizaji wa jeshi la Myanmar na Mabudha wa nchi hiyo dhidi ya Waislamu wa Rohingya na kuwafanya wakimbilie katika nchi jirani ya Bangladesh. Hivi sasa pia kambi hizo zina hali mbaya sana kufuatia kuongezeka idadi ya wakimbizi. 
Waislamu wa Rohingya zaidi ya laki tano wamelazimika kukimbilia Bangladesh kutokana na machafuko na ukandamizaji wa jeshi la Mabudha wenye misimamo mikali dhidi ya jamii hiyo ya waliowachache katika mkoa wa Rakhine magharibi mwa nchi hiyo. 

No comments:

Post a Comment