Wednesday, October 18, 2017

ISRAEL YAPATWA NA PRESHA BAADA YA VISIMA VYOA MAFUTA VYA KIRKUK KUDHIBITIWA NA RERIKALI YA BAGHDAD

Israel yapatwa na presha baada ya visima vya mafuta vya Kirkuk kudhibitiwa na serikali ya Baghdad
Kiongozi wa eneo la Kurdistan Iraq anayechochewa na Israel kujitenga
Utawala haramu wa Kizayuni wa Israel umekumbwa na wasi wasi na wahka mkubwa kutokana na Wakurdi kuondolewa katika visima vya mafuta vya eneo la Kirkuk na kisha kudhibitiwa na jeshi la serikali kuu ya Iraq.
Visima vya mafuta vya eneo hilo, ndivyo vilivyokuwa vyanzo vikuu vya kudhamini mafuta ya utawala haramu wa Israel kutokea Kurdistan. Habari zaidi zinaeleza kuwa, kusonga mbele jeshi la Iraq katika mji wa Kirkuk na kudhibitiwa visima hivyo, kumeutia khofu kubwa utawala wa Kizayuni kwa kuwa hatua hiyo inahatarisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa Tel Aviv.
Kanali ya Pili ya televisheni ya Israel sambamba na kuthibitisha habari hiyo imetangaza kuwa, visima vya mafuta vilivyodhibitiwa na jeshi la Iraq katika eneo la Kirkuk vilikuwa chanzo kikuu cha kudhaminiwa mafuta ya Israel. Ehud Yarri, mchambuzi mashuhuri wa Israel ameiambia kanali hiyo ya Kizayuni kwamba, mji wa Kirkuk wa Iraq, ni moja ya miji tajiri ya mafuta na muhimu sana kwa Iraq na kwamba jeshi la serikali ya Baghdad limeweza kuudhibiti mji huo bila ya vita. Mafuta ya eneo la Kurdistan nchini Iraq yalikuwa yanasafirishwa kwenda Israel kupitia mipaka ya Uturuki.
Jeshi la Iraq lilipodhibiti mambo huko la Kirkuk
Kwa mujibu wa duru za kuaminika, nusu nzima ya mafuta yaliyokuwa yakichimbwa katika visima vya mafuta vya eneo la Kirkuk mwaka 2017 ilitumwa kwenda Israel na ilikuwa ni mapipa laki tatu kwa siku. Ni kwa ajili hiyo ndio maana utawala wa Kizayuni wa Israel ulikuwa ukilichochea eneo la Kurdistan kujitenga na serikali kuu ya Baghdad.

No comments:

Post a Comment