Saturday, October 28, 2017

BURUNDI YACHUKUA HATUA YA KUREFUSHA KIPINDI CHA URAIS WA NKURUNZIZA

Burundi yachukua hatua ya kurefusha kipindi cha urais wa Nkurunziza
Baraza la mawaziri la Burundi limeunga mkono mabadiliko ya katiba ambayo yatamruhusu rais wa sasa wa nchi hiyo kubakia madarakani hadi mwaka 2034, suala ambalo limeitumbukiza zaidi nchi hiyo katika mgogoro wa kisiasa.
Afisa mmoja wa ngazi ya juu wa serikali ya Bujumbura amewaambia waandishi habari kuwa baraza la mawaziri limepitisha rasimu ya sheria ya kurekebisha katiba.
Marekebisho yaliyopendekezwa yanataka kuondolewa kikomo cha muda wa mihula miwili na kuongeza muda wa urais kuwa miaka saba.
Iwapo mapendekezo hayo yatapasishwa na Bunge la Burundi kiongozi wa sasa wa nchi hiyo anaweza kubakia madarakani hadi mwaka 20134.
Maafisa wa serikali ya Burundi wanasema kuwa, wataitisha kura ya maoni ya kupasisha mapendelekezo hayo hapo mwakani.
Kambi ya upinzani nchini Burundi umepinga muswada huo ambao inasema umetayarishwa kwa siri kwa shabaha ya kumbakisha Mkurunzinza madarakani.
Makamu mwenyekiti wa chama cha upinzani cha FRODEBU, Leonce Ngendakumana amekosoa vikali hatua hiyo akisisitiza kuwa marekebisho ya katiba hayapasi kufanyika katika anga ya mivutano na ukosema wa amani.
Machafuko ya ndani Burundi yamesababisha vifo vya raia wasio na hatia
Burundi imekumbwa na machafuko ya ndani tangu mwezi Aprili mwaka 2015 wakati kiongozi wa sasa wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza alipotangaza kuwa atagombea tena kiti cha rais. Mamia ya watu wameuawa na maelfu ya wengine wamelazimika kuwa wakimbizi kutokana na machafuko ya ndani.  

No comments:

Post a Comment