Wednesday, October 18, 2017

MMOJA WA VIONGOZI WA TUME YA UCHAGUZI YA IEBC NCHINI KENYA AJIUZULU

Mmoja wa viongozi wa Tume ya Uchaguzi ya IEBC nchini Kenya ajiuzulu
Mmoja kati ya viongozi wanane wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) nchini Kenya ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huo mapema leo Jumatano.
Akitangaza hatua yake hiyo Roselyn Akombe amesema kuwa amechukua uamuzi huo kutokana kwamba hana imani iwapo IEBC inaweza kusimamia uchaguzi wa tarehe 26 ya mwezi huu au la. Amesema kuwa hataki kushuhudia fedheha ya kile kitakachofanyika baada ya uchaguzi. Kadhalika Roselyn Akombe amesema kuwa, kwa kuzingatia kwamba maisha ya Wakenya yako hatarini, ameamua kujiuzulu wadhifa wake kama mmoja wa viongozi wa IEBC. 
Hali ya kisiasa nchini Kenya kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa marudio wa tarehe 26 Oktoba
Akombe amebainisha kwamba Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka ya Kenya (IEBC) ni moja ya vyanzo vya mgogogro wa hivi sasa nchini humo na kwamba tume hiyo imedhibitiwa na pande ambazo hata hivyo hakuzitaja. Baada ya mahakama ya kilele kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa duru ya kwanza uliofanyika tarehe nane Agosti mwaka huu, kiongozi wa upinzani anayewakilisha muungano wa NASA alitaka kuondolewa viongozi wote wa IEBC akisema kuwa hana imani nao tena.

No comments:

Post a Comment