Friday, October 13, 2017

IRAN ITATOA JIBU LINALOFAA KWA UADUI WA MAREKANI

Iran itatoa jibu linalofaa kwa uadui wa Marekani
Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa ya Tehran ameashiria kufanyika kura ya maoni ya kujitenga eneo la Kurdistan la Iraq na kusema kuwa, adui amegonga mwamba katika njama yake ya kuunda kile kinachodaiwa kuwa ni 'Mashariki ya Kati Mpya.'
Ayatullah Mohammad Ali Movahedi Kermani, amesema hayo katika khutba zake za Sala ya Ijumaa hii leo hapa mjini Tehran na amemshauri Masoud Barzani, rais wa eneo lenye mamlaka ya ndani ya Kurdistan nchini Iraq afungamane na serikali kuu ya Baghadad na awaombe radhi watu wa Iraq na pia asiandae uwanja wa utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa na ushawishi katika eneo hili.
Ayatullah Kermani amamuenzi marehemu Jalal Talibani aliyekuwa rais wa Iraq ambaye aliaga duniani tarehe tatu mwezi huu wa Oktoba na kusema: "Talibani daima alikuwa anatafakari kuhusu uhuru, heshima na adhama ya Wairaqi wa kaumu zote."
Sala ya Ijumaa Tehran
Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran pia ameashiria uadui wa Marekani dhidi ya Iran na kuongeza kuwa: "Hotuba ya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya Iran imedhihirisha tena uadui wa Marekani dhidi ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu."
Ayatullah Kermani ameendelea kusema kuwa, wananchi wa Iran kamwe hawatasahau usaliti wa Marekani na kwamba wakuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran watatoa jibu linalofaa kwa uadui wa dola hilo la kibeberu.
Kabla ya khutba za Sala ya Ijumaa, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurusbiha Madhehebu za Kiislamu, Ayatullah Mohsen Araqi alizungumza na waumini na kusema, Ahul Bayt wa Mtume SAW ni msingi wa umoja na mshikamano wa umma mzima wa Kiislamu.

No comments:

Post a Comment