Thursday, October 5, 2017

MAHAKAMA YA KATIBA UHISPANIA YAFUTA KIKAO CHA BUNGE LA CATALONIA

Mahakama ya Katiba Uhispania yafuta kikao cha Bunge la Catalonia
Mahakama ya Katiba ya Uhispania imefuta kikao kilichokuwa kimepangwa kufanywa na Bunge la eneo la Catalonia kwa ajili ya kutangaza rasmi kujitenga eneo hilo.
Uamuzi huo wa kuzuia kikao cha Bunge la Catalonia kilichopangwa kufanyika siku ya Jumatatu Ijayo umechukuliwa kutokana na wito wa baadhi ya vyama vya siasa vilivyoitaka Mahakama ya Katiba ya Uhispania kuchukua uamuzi wa haraka.
Mahakama hiyo imemtahadharisha Spika wa Bunge la Catalonia, Carme Forcadell kwamba atakabiliwa na mashtaka ya jinai iwapo atapuuza uamuzi huo.
Awali mahakama hiyo ilipinga suala la kuitishwa kura ya maoni ya kujitenga eneo la Catalonia huko Uhispania ikilitaja kuwa ni kinyume na katiba. Hata hivyo viongozi wa eneo hilo walipuuza uamuzi huo na kuitisha kura hiyo ambayo imeonesha kuwa, asilimia 92 wa wakazi wa Catalonia wanaunga mkono suala la kujitenga na Uhispania. 
Wacatalani wanataka kujitenga na Uhispania
Waziri Mkuu wa Uhispania, Mariano Rajoy amemtaka kiongozi wa eneo la Catalonia, Carles Puigdemont  kutupilia mbali fikra ya kujitenga eneo hilo la sivyo atakabiliwa na "shari kubwa zaidi".

No comments:

Post a Comment