Friday, October 20, 2017

POLISI KENYA: WATU 4 WAMEUAWA KATIKA MAPAMBANO YA UPINZANI

Polisi Kenya: Watu 4 wameuawa katika maandamano ya upinzani
Polisi ya kenya imesema kuwa watu wanne wameuawa katika maandamano ya upinzani nchini humo katika kipindi cha wiki mbili zilizopita huku uchaguzi wa rais wa marudio ukikaribia kufanyika wiki ijayo. Polisi ya Kenya imesema kuwa watu hao waliuawa katika mapigano yaliyotokea kati ya maafisa polisi na waandamanaji.
Polisi imeeleza kuwa, watu hao waliaga dunia kati ya tarehe 2 mwezi huu na siku ya Jumatatu iliyopita.
Itakumbukwa kuwa, mapema wiki hii Shirika la Msamaha Duniani (Amnesty International) liliituhumu polisi ya Kenya kuwa imeuwa watu 67 katika maandamano ya upinzani yaliyofanywa siku kadhaa baada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliofanyika Agosti nane.
Mapambano ya polisi yasababisha kuuliwa waaandamanaji wafuasi wa upinzani 
Mahakama ya Juu ya Kenya ilitengua ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta ikisema kuwa uchaguzi wa rais uligubikwa na kasoro na kuagiza uchaguzi wa marudio. Kiongozi wa muungano wa upinzani (Nasa) Raila Odinga ambaye hoja yake ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa rais mahakamani ilipelekea kutenguliwa matokeo ya uchaguzi huo, ametangaza kujitoa katika uchaguzi wa marudio akisema kuwa uchaguzi huo una hatari ya kugubikwa na kasoro kama zile zilizojitokeza katika uchaguzi uliopita.

No comments:

Post a Comment