Thursday, October 5, 2017

JUMUIYA ZA KUTETEA HAKI ZA BINADAMU ZAIPONGEZA UN KWA KUIWEKEA SAUDIA KATIKA ORODHA NYEUSI

Jumuiya za kutetea haki za binadamu zaipongeza UN kwa kuiweka Saudia katika orodha nyeusi
Jumuiya za kimataifa za kutetea haki za binadamu zimepongeza hatua ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ya kuiweka Saudi Arabia na washirika wake katika orodha nyeusi ya nchi na jumuiya zinazokiuka haki za watoto katika maeneo yenye vita.
Mkurugenzi wa kitengo cha watoto katika shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, Jo Becker amesema kuwa, uamuzi wa kuiweka Saudi Arabia katika orodha nyeusi ya UN unapaswa kufuatiwa na hatua za kivitendo za kuhakikisha kwamba, Riyadh na washirika wake wanaheshimu sheria za kuwalinda watoto. Becker amesisitiza kuwa, umewadia wakati wa muungano unaoongozwa na Saudia kukomesha kikamilifu mashambulizi yake dhidi ya watu wa Yemen.
Wakati huo huo mwakilishi wa shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York amesema shirika hilo limefurahi kuona Antonio Guterres akifanya yaliyomshinda katibu Mkuu wa kabla yake wa Umoja wa Mataifa baada ya kuona kuwa, idadi kubwa ya watoto wameuawa katika mashambulizi ya Saudia na washirika wake huko Yemen.
Uharibifu mkubwa wa mashambulizi ya Saudia na washirika wake Yemen
Sherine Tadros amesisitzia kuwa, kuna ulazima wa kuwekwa marufuku ya kuiuzia silaha Saudi Arabia na washirika wake katika vita dhidi ya watu wa Yemen.
Mamia ya watoto wadogo wameuawa, shule, hospitali na miundombuni kuvunjwa kabisa katika mashambulizi yanayofanywa na Saudi Arabia na washirika wake dhidi ya Yemen yanayoendelea kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

No comments:

Post a Comment