Wednesday, October 18, 2017

UGANDA YAPIGA MARUFUKU MAANDAMANO YA KUPINGA KUONDOLEWA KIPENGELE CHA UMURI KATIKA KATIKA KUGOMBEA URAIS

Kiongozi wa upinzani, Daktari Kiiza Besigye akipandishwa kwenye gari la polisi baada ya kusambaratishwa maandamano Kiongozi wa upinzani, Daktari Kiiza Besigye akipandishwa kwenye gari la polisi baada ya kusambaratishwa maandamano
Jeshi la polisi nchini Uganda leo (Jumatano) limepiga marufuku kile lilichokiita ni maandamano haramu ya kupinga mpango wa kuondoa kipengee ya umri katika kugombea urais. Juhudi za kuondoa kipengee hicho zina nia ya kumfungulia njia Rais Yoweri Museveni kuendelea kubakia madarakani bila ya kufungwa na kipengee hicho.
Muswada wa kuondoa kipengee cha umri wa kugombea urais kiliwasilishwa katika bunge la Uganda mwezi uliopoita na hivi sasa wabunge wanajadiliana na wananchi wa kawaida kutaka kujua maoni yao. Hata hivyo juhudi hizo zimekumbwa na upinzani kutoka sehemu mbalimbali.
Rais Yoweri Museveni wa Uganda

Msaidizi wa Inspekta Mkuu wa Polisi wa Uganda, Assuman Mugenyi amesema kuwa, majadiliano hayo yanaruhusiwa lakini si ruhusa kufanya maandamano yasiyo na kibali, kuchochea machafuko, kufanya kampeni za chuki, kutumia maneno ya kashfa na vitu kama hivyo.
Kwa kawaida wapinzani hawapewi vibali vya kuandamana nchini Uganda na hii ina maana kwamba maandamano yoyote ya wapinzani ni kinyume cha sheria.
Musenyi ametoa amri kwa maafisa wa polisi kuhakikisha kuwa wabunge wanafanya mashauriano hayo kwa utulivu na amani tena katika majimbo yao tu.
Jana usiku, polisi walifyatua mabomu ya kutoa machozi na kutumia risasi za plastiki kutawanya mamia ya wapinzani wa kufutwa kipengee cha umri kinachomzuia Museveni kugombea tena urais.
Winnie Kiiza, Mkuu wa Mrengo wa Upinzani katika bunge la Uganda

Rais Yoweri Kaguta Museveni amekuwa akiitawala Uganda kwa miaka 30 sasa. Umri wake hivi sasa ni miaka 73 wakati katiba ya Uganda imepiga marufuku mtu kugombea urais akiwa na umri wa miaka 75.
Mkuu wa mrengo wa upinzani katika bunge la Uganda, Winne Kiiza amesema kuwa, amri hiyo ya polisi ni kinyume cha katiba na ameahidi kukabiliana na amri hiyo kwa njia yoyote ile.
Hadi hivi sasa haijajulikana muswada huo utarejeshwa lini Bungeni kwa ajili ya kupigiwa kura.

No comments:

Post a Comment