Thursday, November 16, 2017

WAMAREKANI WAZIDI KUPIGANA RISASI KIHOLELA, MAKUMI WAUAWA NA KUJERUHIWA

Wamarekani wazidi kupigana risasi kiholela, makumi wauawa na kujeruhiwa
Watu 16 wameuawa na wengine 24 kujeruhiwa katika matukio 56 ya kupigana risasi kiholela yaliyotokea katika kipindi cha masaa 24 kwenye maeneo tofauti ya Marekani.
Kituo cha kutoa takwimu za mashambulizi ya silaha nchini Marekani kimetangaza habari hiyo na kuongeza kuwa mauaji na mashambulizi hayo yametokea katika kipindi cha masaa 24 yaliyopoita katika majimbo ya Florida, Michigan, Texas, Ohio na Pennsylvania. 
Kwa mujibu wa kituo hicho cha Marekani, katika kipindi cha masaa 48 yaliyopita, kumeripotia matukio 164 ya kupigana risasi kiholela katika kona mbalimbali za Marekani ambayo yamepelekea watu 45 kuuawa na wengine 88 kujeruhiwa.
Umilikaji silaha ovyo, mgogoro mkubwa kwa Marekani

Takwimu zinaonesha kuwa, jamii ya Marekani ndiyo yenye silaha nyingi zaidi zinazomilikiwa na watu majumbani kuliko jamii nyingine yoyote duniani kiasi kwamba kati ya kila watu 100, 90 kati yao wana silaha nyepesi majumbani mwao.
Takwimu zinaonesha pia kuwa makundi ya utengenezaji silaha yana nguvu sana nchini Marekani na ndiyo yanayodhibiti vyama vya Democrats na Republican, hivyo serikali yoyote inayoingia madarakani haina nguvu ya kupiga marufuku umilikaji silaha ovyo nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment