Saturday, November 25, 2017

MAREKANI YAUNGA MKONO JINAI ZA SAUDIA DHIDI YA RAIA WA YEMEN

Marekani yaunga mkono jinai za Saudia dhidi ya raia wa Yemen
Ikulu ya Rais wa Marekani, White House, imetangaza kuunga mkono jinai za utawala wa Saudi Arabia dhidi ya Yemen.
Katika taarifa siku ya Ijumaa, White House, pasi na kuashiria indhari za taasisi za kimataifa kuhusu nafasi ya Marekani na muitifaki wake , Saudia, katika kuleta maafa ya kibinadamu nchini Yemen, kwa mara nyingine ilitangaza uungaji mkono wa Washington kwa Saudia na waitifaki wake katika vita dhidi ya Yemen.
Taarifa ya Ikulu ya White House, kinyume na ukweli wa mambo, ilidai kuwa utawala wa Saudia umefungua Bandari ya Al Hudayda na Uwanja wa Ndege wa Sanaa.
Utawala wa Riyadh,ambao unadhibiti mipaka yote ya kimatiafa ya Yemen, ulikuwa umeahidi kufungua Bandari ya Hudayda na Uwanja wa Ndege wa Sanaa baada ya kufunga maeneo hayo mawili 24 Novemba na kwa msingi hiyo kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia katika eneo hilo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Dunaini, WFP, limeonya kuwa mamilioni ya watu wa Yemen wanakabiliwa na hatari ya mauti kufuatia mzingiro uliowekwa na Saudi Arabia dhidi ya nchi hiyo na hivyo kuzuia misaada kuwafikia wanaohitajia.
Watoto ni waathirika wa jinai za Saudia nchini Yemen
Saudia ilianzisha hujuma yake dhidi ya Yemen mnamo Machi mwaka 2015 kwa uungaji mkono wa Marekani kwa lengo la kuirejesha madarakani serikali kibaraka ya Abdu Rabuh Mansour Hadi aliyejiuzulu urais na kukimbilia mji mkuu wa Saudia, Riyadh. Hivi sasa Saudia inzuia misaada kuwafikia mamilioni ya watu wa nchi hiyo wanaokabiliwa na njaa.
Raia zaidi ya elfu 13  wa Yemen wameuawa, hasa wanawake na watoto, na maelfu ya wengine kujeruhiwa katika uvamizi huo wa kijeshi huku Umoja wa Mataifa ukishindwa kuchukua hatua yoyote ya kuzuia jinai hizo za Saudia huko Yemen. Aidha watu zaidi ya laki sita wameambukizwa ugonjwa wa kipindupindu kote Yemen huku wengine zaidi ya 2,000 wakifarikia dunia tokea mwezi Aprili mwaka huu.

No comments:

Post a Comment