Wednesday, November 8, 2017

AMISOM KUONDOA ASKARI 1,000 NCHINI SOMALIA

AMISOM kuondoa askari 1,000 nchini Somalia
Ujumbe wa Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) umetangaza kuwa utaondoa askari 1,000 kutoka Somalia hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.
Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika nchini Somalia, Francisco Madeira amesema kuwa AMISOM imeanza kupunguza idadi ya askari wake nchini humo na kwamba kufikia tarehe 31 Disemba askari 1000 wa kikosi hicho watakuwa wameondoka katika ardhi ya Somalia.
Madeira amesisitiza umuhimu wa kuwepo umoja kati ya raia na jeshi nchini Somalia dhidi ya ugaidi na kusema jeshi peke yake haliwezi kuwashinda magaidi bila ya msaada ya raia. Amewataka Wasomalia wote kushirikiana kwa ajili ya kuwafukuzia mbali wapiganaji wa kundi la kigaidi la al Shabab. 
Kikosi cha majeshi ya Umoja wa Afrika cha AMISOM ambacho kiliundwa kupitia azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kimekuwa kikiisaidia serikali ya Somalia kupambana na magaidi wa kundi la al Shabab tangu mwaka 2007. 
Askari wa kikosi cha AMISOM, Somalia
Kikosi hicho kinaundwa na askari elfu 22 kutoka nchi za Uganda, Kenya, Djibouti, Burundi na Ethiopita.
Magaidi wa al Shabab wamezidisha mashambulizi ya kujilipua kwa mabomu katika wiki za hivi karibuni husuan katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu. 

No comments:

Post a Comment