Wednesday, November 15, 2017

RUSSIA YATAHADHARISHA KUHUSU HATUA YA MAREKANI KWA VYOMBO VYAKE VYA HABARI

Russia yatahadharisha kuhusu hatua ya Marekani kwa vyombo vyake vya habari
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia ametangaza kuwa kila hatua itakayochukuliwai na Marekani dhidi ya waandishi habari na vyombo vya habari vya Russia haitaachwa bila ya jibu.
Dmitry Peskov amesema kuwa hatua yoyote itakayopelekea kubanwa uhuru wa vyombo vya habari vya Russia nje ya nchi haitasalia bila ya jibu; na kwamba hatua hiyo itafuatiliwa pia na fikra za waliowengi na kwa njia za kisheria.  
Dmitry Peskov, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia 
Katika fremu hiyo, Bunge la Russia (Duma) limepasisha mswada dhidi ya vyombo vya habari vya Marekani vinavyoendesha shughuli zake huko Russia. Bunge la Russia limetangaza kuwa, limechukua hatua hiyo kama jibu kwa hatua za karibuni za Marekani dhidi ya Televisheni ya Russia Today. Mwanasheria Mkuu wa Marekani siku kadhaa zilizopita aliitaka televisheni hiyo ya Russia Today iwe imejisali kama taasisi ya kigeni hadi kufikia tarehe 13 mwezi huu; kinyume chake akaunti za fedha za televisheni hiyo zilizopo Marekani zitafungwa.

No comments:

Post a Comment