Sunday, November 26, 2017

KILA SIKU WANAWAKE 600 HUFANYIWA VITENDO VYA UKATILI NCHINI MAREKANI

Kila siku wanawake 600 hufanyiwa vitendo vya ukatili nchini Marekani
Vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake katika nchi za Magharibi na hasa Marekani vimefikia kiwango cha kutia wasiwasi kinyume na inavyodaiwa huku ikiripotiwa kwamba kila siku wanawake 600 hufanyiwa vitendo vya ukatili nchini humo.
Kwa mujibu wa shirika la habari la IRNA jitihada nyingi zinafanywa na makundi na asasi mbalimbali ili kupunguza kiwango cha vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake nchini Marekani lakini takwimu za mauaji, ubakaji na unyanyasaji dhidi ya wanawake nchini humo zinatia wasiwasi.
Wanaharakati wa haki za binadamu nchini Marekani wanaitakidi kuwa nchi hiyo sio tu inapaswa kuziangalia upya sheria zake kuhusu ukatili dhidi ya wanawake, watoto wadogo wa kike na hata wa kiume lakini pia inatakiwa izingatie na kulipa umuhimu zaidi suala la usalama katika mazingira ya kazi, maskulini, makanisani, kwenye kambi za jeshi pamoja na klabu za michezo na burudani.
Wakati huohuo ripoti kutoka nchini Marekani zinaeleza kuwa bunge la nchi hiyo linaandaa mpango kwa ajili ya wafanyakazi wake wa kike ili waweze kukabiliana na ubakaji na vitendo vya ukatili vinavyowaandama.
John Conyers
Ripoti hiyo imekumbusha kuwa katika kipindi cha chini ya mwezi mmoja, shakhsia kadhaa maarufu wa kisiasa, wa tasnia ya filamu, michezo na vyombo vya habari wamekabiliwa na tuhuma za kuwanyanyasa kijinsia wanawake.
Hayo yanajiri huku John Conyers, mkuu wa kamati ya vyombo vya mahakama ya Baraza la Wawakilishi la Marekani akitangaza kujiuzulu wadhifa wake huo kutokana na kashfa ya masuala ya maadili.../

No comments:

Post a Comment