Monday, January 29, 2018

RAILA ODINGA KUAPISHWA KESHO JUMANNE JAN.30 2018.

   Picha inayohusiana
Kiongozi wa mungano wa upinzani nchini Kenya NASA, Raila Odinga anatarajiwa kuapishwa kama rais wa Jamhuri ya Kenya January 30, 2018 Kuapishwa huko kunatokana na upinzani nchini Kenya kutokukubaliana na ushindi wa rais Uhuru Kenyatta aliyechaguliwa mwishoni mwa mwaka uliopita, ingawa upinzani haukushiriki duru ya pili ya uchaguzi baada ya matokeo ya uchaguzi wa awali kukataliwa na mahakama.
Hata hivyo baadi ya wafuasi wa NASA hawaungi mkono hatua hiyo. Pia wafuasi wa chama tawala cha Jubilee wanapinga vikali kuapishwa kwa Raila Odinga kwa kudai kuwa huenda machafuko yakatokea.
Tukio la kuapishwa kwa Odinga pia linapingwa vikali na Wakenya waishio nje ya nchi hiyo. Kwa upande wa jeshi la polisi nchini Kenya limeimarisha usalama mjini Nairobi katika eneo lililoteuliwa kwa ajili ya tukio hilo la kipekee, na kusisitiza kuwa hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kwenda eneo hilo, ingawa wafuasi wengine wa NASA wanaandaa usafiri wa kuelekea maeneo ya Nairobi kushuhudia sherehe za kuapishwa kwa Odinga.

No comments:

Post a Comment