Thursday, January 11, 2018

ASKARI WA COTE D'LVOIRE WAENDELEZA UASI LICHA YA MKUU WA JESHI KUWAOMBA RADHI

Askari wa Côte d’Ivoire waendeleza uasi licha ya mkuu wa jeshi kuwaomba radhi
Askari wa Côte d’Ivoire wameendeleza ghasia licha ya mkuu wa majeshi ya nchi hiyo kuwaomba radhi.
Duru za habari nchini humo zimetangaza kwamba, mapigano ya siku kadhaa zilizopita kati ya makundi ya jeshi, yamepelekea askari kadhaa kuuawa na wengine kujeruhiwa.
Ghasia nchini za asjari Côte d’Ivoire
Inafaa kuashiria kwamba miezi michache iliyopita kuliibuka uasi wa askari katika mji wa Bouaké nchini Ivory Coast kutokana na matatizo ya kiuchumi na kushindwa serikali kulipa madai ya wafanyakazi na askari, matatizo ambayo yalienea pia katika maeneo mengine ya Côte d’Ivoire.
Akiwa na Rais Alassane Ouattara, Mkuu wa Mmajeshi nchini humo aliomba radhi kwa taifa kutokana na uasi wa askari hao waliochafua usalama huku akiahidi kufanyika marekebisho jeshini katika mwaka mpya. Uasi wa zamani ambao uliwajumuisha pia askari ambao walikuwa wanataka kulipwa marupurupu yao, ulishika kasi zaidi mwezi Januari na mwezi Mei mwaka jana na kuisababishia matatizo makubwa serikali ya Yamoussoukro.
Rais Alassane Ouattara wa nchi hiyo
Karibu askari 1000 mwaka jana waliachishwa kazi jeshini katika fremu ya marekebisho hayo. Mwaka 2011 Côte d’Ivoire ilikumbwa na vita vya ndani ambapo baada ya makubaliano, askari kadhaa waasi walijiunga na jeshi ambapo kwa mujibu wa viongozi wa serikali, askari hao ndio wamekuwa chanzo cha uasi tangu mwaka jana hadi sasa.

No comments:

Post a Comment