Sunday, January 7, 2018

WATU 32 WATOWEKA KATIKA AJALI YA MELI MASHARIKI MWA PWANI YA CHINA

Watu 32 watoweka katika ajali ya meli mashariki mwa pwani ya China
Raia 30 wa Iran na wawili wa Bangladesh wameripotiwa kutoweka baada ya meli ya mafuta na nyingine ya mizigo kugongana mashariki mwa pwani ya China.
Wizara ya Uchukuzi ya China imesema meli ya mafuta ya Iran yenye jina 'Sanchi' imegongana na meli ya mizigo yenye nambari ya usajali ya Hong Kong inayoitwa “CF Crystal” mashariki mwa bahari ya China katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia leo.
Taarifa ya wizara hiyo imesema meli hiyo ya mizigo ya China iliyokuwa na mabaharia 21 ilikuwa imebeba tani 64,000 za nafaka na ilikuwa ikitokea Marekani kuelekea katika mkoa wa Guangdong nchini China.
Meli ya mafuta iliyoripuka
Wizara ya Uchukuzi ya China imesema mabaharia wake wote waliokuwa katika meli hiyo ya mizigo wameokolewa.   
Habari zaidi zinasema kuwa, meli ya mafuta ambayo ilikuwa imebeba tani 136,000 za mafuta kwa ajili ya Korea Kusini iliripuka na kuteketea katika ajali hiyo.
Shirika rasmi la habari la Iran (IRNA)  limethibitisha kuwa meli hiyo ya mafuta ni milki ya nchii hii lakini ilikuwa imekodiwa na shirika moja la Korea Kusini.
Polisi ya Baharini ya Korea Kusini inaongoza katika operesheni ya uokoaji na kutafuta miili ya walipoteza maisha katika ajali hiyo.

No comments:

Post a Comment