Monday, January 29, 2018

MAANDAMANO YAENDELEA ETHIOPIA, VIFO VYARIPOTIWA.

Tokeo la picha la ETTIOPIA STRIKES
Wakati mkutano wa kilele wa viongozi wa Umoja wa Afrika AU, ukiendelea mjini Addis Ababa Ethiopia chini ya mwenyekiti wa Umoja huo Paul Kagame, kwa upande mwingine Maandamano yameripotiwa na vyombo vya habari nchini humo ambapo watu kadhaa wameripotiwa kuuwawa katika ghasia hizo zilizofanyika kaskazini mwa nchi hiyo.
Barabara zinaelezwa kuwa ziliwekwa vizuizi huku majengo ya serikali yakielezwa kushambulia. Maandamano hayo yalianza wiki iliyopita baada ya majeshi ya serikali kushambulia waumini wakati wa sherehe za kidini katika mji wa Weldiya, na kusababisha vifo vya watu watano.
Hivi karibuni serikali ya Ethiopia ilitoa uamuzi wa kuwaachia huru maelfu ya wanaharakati, uamuzi ambao haukutuliza maandamanao hayo, ambayo yamekuwa yakifanyika karibu miaka mitatu sasa.

No comments:

Post a Comment