Wednesday, January 24, 2018

PAPA ATOA WITO WA KUPIGWA VITA UBAKAJI NA KUNAJISIWA WATOTO

Papa atoa wito wa kupigwa vita ubakaji na kunajisiwa watoto
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesisitiza juu ya ulazima wa kuchukuliwa hatua za dhati za kukabiliana na vitendo vya ubakaji na kunajisiwa watoto.
Papa Francis amesema hayo baada ya kurejea kutoka katika safari yake ya Amerika ya Latini ambayo iligubikwa na kashfa za ngono katika makanisa ya katoliki.
Sambamba na kutahadharisha kuhusiana na vitendo vya kubakwa na kunajisiwa watoto wadogo amesisitiza kwamba,  wahusika wanapaswa kuchukuliwa hatua.
Itakumbukwa kuwa, akiwa katika safari yake nchini Chile, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani alieleza masikitiko yake kutokana na kashfa za ngono na ulawiti zinazolikabili kanisa hilo nchini humo.
Papa Francis akiwasili Bangladesh
Katika hotuba yake ya kwanza akiwa pamoja na Rais Michelle Bachelet wa Chile, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani alisema kuwa, kashfa hizo za ngono zimelipaka matope kanisa hilo.
Kashfa mbalimbali za kimaadili na kifedha zilizoikumba Vatican na Kanisa Katoliki katika miaka ya hivi karibuni zimekuwa zikigonga vichwa vya habari na kuwa gumzo kubwa lisilokwisha duniani. 
Kuna mamia ya kesi za ubakaji na ulawiti zinazowakabili makasisi wa kanisa hilo, ambazo zimerundikana katika mahakama za Ulaya na Marekani zikisubiri kufanyiwa uchunguzi, jambo ambalo limeshusha hadhi ya Kanisa Katoliki Duniani.

No comments:

Post a Comment