Sunday, January 28, 2018

MKUTANO WA WAKUU WA AFRIKA UNAENDELEA MJINI ADDIS ABABA, ETHIOPIA

Mkutano wa wakuu wa Afrika unaendelea mjini Addis Ababa, Ethiopia
Mkutano wa 32 cha Umoja wa Afrika (AU) umeanza huko Addis Ababa mji mkuu wa Ethiopia kwa kuhudhuriwa na viongozi wengi wa nchi za Kiafrika.
Vikao vya duru ya 32 ya Mkutano wa Umoja wa Afrika vimeanza leo Jumapili kwa kuhudhuriwa na viongozi wengi wa nchi za Afrika. Vikao hivyo vimeendeshwa katika hali ya faragha na duru ya 32 ya Mkutano wa Viongozi wa Afrika imepangwa kufunguliwa baada ya kumalizika vikao hivyo.   
Duru ya 32 ya Mkutano wa Viongozi wa Nchi za Afrika waanza Addis Ababa
 
Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye anahudhuria katika mkutano huo amesisitiza kuwa ipo haja ya kuungwa mkono nchi za bara la Afrika ili kuweza kuwa na amani na kustawisha taasisi za nchi hizo. Guterres amesema kuwa, askari jeshi wa Umoja wa Mataifa wataendelea na shughuli zao barani Afrika. 
Duru ya 32 ya Mkutano wa Viongozi wa Nchi za Afrika itadumu kwa siku mbili; ambapo washiriki katika mkutano huo watajadili na kuchunguza  mizozo na changamoto kuu zinazozikabili baadhi ya nchi za Afrika, ugaidi, na suala la kuimarisha mashirikiano kati ya nchi hizo chini ya kaulimbiu "Ushindi katika mapambano dhidi ya ufisadi na mageuzi Afrika."

No comments:

Post a Comment