Monday, January 29, 2018

CHINA YAKANUSHA KUFANYA UJASUSI KATIKA MAKAO MAKUU YA AU

China yakanusha kufanya ujasusi katika Makao Makuu ya AU
Balozi wa China katika Umoja wa Afrika AU amekanusha vikali madai ya vyombo vya habari vya Magharibi vilivyodai kuwa nchi hiyo inafanya ujasusi katika Makao Makuu ya AU mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Kuang Weilin amesema kuwa madai ya gazeti la Ufaransa la Le Monde ya kwamba nchi yake inafanya ujasusi katika Makao Makuu ya AU mjini Addis Ababa tangu mwaka 2012 hadi 2017 ni ya kipuuzi na hayana ukweli wowote.
Makao Makuu ya AU mjini Addis Ababa, Ethiopia

Balozi huyo wa China amesema hayo pambizoni mwa kikao cha wakuu wa Umoja wa Afrika kilichofanyika Jumapili na Jumatatu tarehe 28 na 29 Januari 2018 katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.
Amesema: "Gazeti hilo la Ufaransa limepoteza heshima yake kwa kusambaza madai hayo ya uongo siku ya Ijumaa na kamwe madai kama hayo hayawezi kuharibu uhusiano wa China na Afrika."
Siku ya Ijumaa gazeti la Le Monde la Ufaransa lilinukuu baadhi ya duru za Umoja wa Afrika zikidai kwamba wataalamu wa kompyuta wamegundua kuwa, kwa muda wa mwaka mzima sasa taarifa za watumizi wa kompyuta wa AU zinapelekwa kwa upande wa tatu ulioko mjini Shanghai, China.
Bendera za nchi za Afrika

Kwa upande wake, Umoja wa Afrika umesema unashughulishwa zaidi na uhusiano imara kati ya Afrika na China kuliko madai hayo ya gazeti la Ufaransa.
Itakumbukwa kuwa China ndiye mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa nchi za Afrika.

No comments:

Post a Comment