Wednesday, January 24, 2018

BARAZA LA USALAMA LINAKUTANA LEO KUJADILI KADHIA YA PALESTINA

  • Baraza la Usalama linakutana leo kujadili kadhia ya Palestina
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linakutana leo Alkhamisi katika kikao chake cha dharura kwa shabaha ya kujadili kadhia ya Palestina.
Tayseer Jaradat, Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Palestina amesema kuwa, kikao hicho cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kinafanyika kwa ombi la Palestina.
Riyadh Mansour, balozi na mwakilishi wa kudumu wa Palestina katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, lengo la kikao hicho ni kulikumbusha majukumu yake Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na Palestina.
Itakumbukwa kuwa, Disemba 21 mwaka jana, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipasisha kwa wingi wa kura azimio la kuiunga mkono Beitul-Muqaddas.
Beitul-Muqaddas, Palestina
Kwa mujibu wa azimio hilo, Umoja wa Mataifa ulitangaza kwamba, hauitaimbua Beitu-Muddas kama mji mkuu wa utawala ghasibu wa Israel.
Tarehe 6 mwezi uliopita wa Disemba, Rais Donald Trump wa Marekani aliitangaza Quds Tukufu kuwa eti ni mji mkuu wa utawala pandikizi wa Israel na akatoa amri ya kufanyika taratibu za kuuhamishia mjini humo ubalozi wa Marekani ulioko Tel Aviv, mji mkuu wa utawala dhalimu wa Kizayuni.
Hii ni katika hali ambayo, mji wa Quds kunakopatikana Masjid Aqswa, kibla cha kwanza cha Waislamu ni sehemu isiyotenganishika na Palestina na ni miongoni mwa maeneo matatu muhimu na matakatifu baada ya Makka na Madina.

No comments:

Post a Comment