Sunday, January 28, 2018

POLISI UJERUMANI YAWATAWANYA WAANDAMANAJI TAKRIBANI 15,OOO

Deutschland | Polizei löst Kurden-Demo in Köln
Chanzo, DW.
Jeshi la Polisi nchini Ujerumani limewatawanya  waandamanaji takribani 15,000 wa kikurdi waliokuwa wamebeba mabango yanayoonesha  nembo  za  chama  cha  wafanyakazi wa  Kikurdi PKK, zilizopigwa marufuku  nchini  humo.
Katika taarifa zilizoripotiwa na shirika la habari la Ujerumani DW, zilieleza kuwa Maandamano  hayo yaliyofanyika mjini Kolon-Ujerumani, yalitayarishwa  na  chama cha wafanyakazi cha NAV-DEM cha Wakurdi  ambacho  kinaelezwa  kuwa na ukaribu na chama kilichopigwa  marufuku  cha  PKK. Chama hicho kinaelezwa pia kupigwa  marufuku nchini Uturuki pamoja na washirika wake wa mataifa  ya magharibi  kwamba ni kundi la kigaidi. Watu  wawili walikamatwa  katika  maandamano  hayo, ambayo yaliyokuja wiki moja baada ya vikosi maalum vya jeshi la Uturuki na waasi ambao ni washirika wa Uturuki nchini Syria, kufanya mashambulizi yakuwalenga wanamgambo wa Kikurdi wa kundi la vikosi vya ulinzi wa umma YPG, kaskazini mwa Syria.
Hakuna  tukio  lililoripotiwa  mara  moja, japo hali iliripotiwa kuendelea kuwa tete, kwa mujibu wa msemaji wa polisi ambaye aliongeza kwamba kulikuwa na wasi wasi juu  yakuzuka mapambano kati ya waandamanaji  na polisi.

No comments:

Post a Comment