Sunday, January 14, 2018

BANDERA ZA ISRAEL ZACHOMWA MOTO KUMKARIBISHA NETANYAHU INDIA

Bandera za Israel zachomwa moto kumkaribisha Netanyahu India
Maandamano makubwa yameshuhudiwa katika mji mkuu wa India, New Delhi, kabla ya kuanza safari ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu katika nchi hiyo.
Makumi ya waandamanaji hao, aghalabu yao wakiwa vijana wa Kiislamu jana Jumamosi waliteketeza moto bendera za utawala wa Kizayuni, kulalamikia safari ya Netanyahu katika nchi yao.
Waandamanaji hao waliokuwa na ghadhabu wamekosoa vikali hatua ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani, ya kuitambua Quds Tukufu kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel.
Baadhi ya vijana hao aidha wamechoma moto mabango yaliyokuwa na picha za Trump na Netanyahu.
Maandamano ya kupinga safari ya Netanyahu India
Duru za habari zinasema kuwa, maandamano kama hayo ya New Delhi yameshuhudiwa katika vijiji zaidi ya elfu moja nchini India.
Netanyahu anatazamiwa kuanza safari ya kikazi ya siku sita nchini India, licha ya New Delhi kupiga kura ya kuunga mkono azimio la Umoja wa Mataifa la kupinga uamuzi wa Marekani wa kuitambu Quds kuwa mji mkuu wa Israel.

No comments:

Post a Comment