Monday, January 8, 2018

UOZO BANDARINI TANZANIA WAMFANYA RAIS MAGUFULI AFANYE MABADILIKO MAPYA YA UONGOZI

Uozo bandarini Tanzania wamfanya Rais Magufuli afanye mabadiliko mapya ya uongozi
Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania ametengua uteuzi wa Kamishna wa Madini Mhandisi Benjamin Mchwampaka na kumteua Profesa Shukrani Manya, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kuwa Kamishna wa Madini nchini humo.
Magufuli ametangaza uteuzi huo Jumatatu ya leo katika hotuba fupi aliyoitoa mara baada ya kumwapisha Dotto Mashaka Biteko kuwa Naibu Waziri wa Madini wanchi hiyo. Katika hotuba hiyo Magufuli amesema: "Mambo ya ovyo ni mengi mno, nilipotembelea bandarini niliunda katume kasirisiri hivi, kwa kulihusisha Jeshi la Wananchi, TISS na Polisi.

Wakati Rais Magufuli alipotembelea bandari ya Dar es Salaam mwishoni mwa mwaka jana
Aidha amesema: "Yanayogundulika huko ni ya ajabu, kuna hadi simenti za zamani sana, yapo makontena bandarini na pale Ubungo." Akielezea kutohitaji kuwabembeleza watendaji wa serikali wanaofanya uzembe rais huyo wa Tanzania amesema: "Mimi si mwanasiasa mzuri wa kubembelezabembeleza, nikitoka mimi mtapata wa kubembeleza, ila mimi nataka kabla ya Ijumaa regulations (kanuni za sheria ya madini) ziwe zimesainiwa. Kadhalika Magufuli ameelezea kutoridhishwa kwake na namna viongozi na watendaji wa Wizara ya Madini wanavyotekeleza majukumu yao polepole na bila ya kujali maslahi ya nchi hiyo mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment