Thursday, January 4, 2018

MAELFU YA WAPAKISTANI WAANDAMANA KUPINGA TUHUMA ZA TRUMP, WATAKA KUTIMULIWA BALOZI WA US

Maelfu ya Wapakistani waandamana kupinga tuhuma za Trump, wataka kutimuliwa balozi wa US
Makumi ya maelfu ya Wapakistani wamefanya maandamano katika miji tofauti ya nchi hiyo katikka kulalamikia matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya nchi yao na wameitaka serikali kumtimua balozi wa Marekani nchini humo.
Maandamano yameshuhudiwa katika miji ya Lahore, Faisalabad, Hyderabad na miji mingine ya kusini mwa nchi hiyo ambapo waandamanaji wamelaani siasa za kichokozi na kupenda kujitanua za Trump dhidi ya mataifa mengine. Kadhalika waandamanaji hao waliokuwa na hasira wamelichoma moto sanamu la rais huyo wa Marekani na pia bendera ya nchi hiyo na kusisitiza azma yao ya kuitaka serikali ya Islamabad kumtimua balozi wa Marekani nchini humo.
David Hale, balozi wa Marekani nchini Pakistan
Hii ni katika hali ambayo Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan hivi karibuni ilimwita balozi wa Marekani nchini humo David Hale katika kulalamikia tuhuma za hivi karibuni za rais wake dhidi ya nchi hiyo. Mahusiano kati ya Pakistan na Marekani yameharibika tangu mwezi Agosti mwaka jana baada ya Trump kuituhumu nchi hiyo kwamba inawaunga mkono magaidi huku akitishia kuikatia misaada ya kifedha.

No comments:

Post a Comment