Monday, January 30, 2017

WATU WANANE WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI MSIKITINI QUEBEC, CANADA

Quebec City
Polisi wamekiri kunao watu wamefariki lakini hawajataja idadi
Watu wanne wameuawa kwenye ufyatulianaji wa risasi katika msikiti mmoja mjini Quebec, Canada.
Ufyatulianaji wa risasi ulitokea katika Kituo cha Kitamaduni cha Kiislamu cha Quebec Jumapili usiku, polisi wamesema.
Kituo hicho kimepakia kwenye ukurasa wake wa Facebook video inayoonesha polisi wakiwa nje ya kitu hicho. Video hiyo imeambatana na ujumbe kwamba "baadhi wamefariki".
Polisi wamesema watu wawili wamekamatwa, lakini hawajatangaza idadi kamili ya waliofariki au kujeruhiwa.
Mtu aliyeshuhudia ameambia shirika la habari la Reuters kwamba watu hadi watatu waliokuwa na silaha wamehusika.
Shirika hilo la habari pia limesema maafisa wa usalama waliokuwa na silaha kali wameonekana wakiingia kwenye msikiti huo.
Gazeti la Le Soleil linasema limepata taarifa kwamba mmoja wa washukiwa ni kijana wa miaka 27 mwenye "jina la asili ya Quebec", na alikuwa na bunduki aina ya AK-47.
Ufyatuaji huo wa risasi umetokea katika msikiti ulio kwenye barabara ya Sainte-Foy, moja ya misikiti miwili inayoendeshwa na kituo hicho cha utamaduni wa Kiislamu.
Shambulio lilitekelezwa wakati wa sala ya jioni.
Polisi wamewakamata watu wawili
Polisi wamewakamata watu wawili
Rais wa msikiti huo Mohamed Yangui, ambaye hakuwa ndani ya msikiti wakati wa shambulio, ameambia Reuters kwamba hajafahamu kufikia sasa idadi ya waliojeruhiwa ingawa wamepelekwa hospitali mbalimbali Quebec.
"Nini kinatendeka hapa? Huu ni unyama," amesema.
Juni mwaka jana, kulipatikana karibu na mlango wa msikiti huo kichwa cha nguruwe kilichokuwa kimefungwa vizuri kama zawadi na kuandikwa "bonne appetit". Waislamu hawali nguruwe.
Kichwa
Kituo hicho kilisema zawadi hiyo ilikuwa "ishara ya chuki"
Waziri Mkuu wa Justin Trudeau ameandika kwenye Twitter kwa Kiingereza na Kifaransa na kusema, "Usiku huu, raia wa Canada wanaomboleza waliouawa kwenye shambulio hili la woga katika msikiti mmoja Quebec. Fikira zangu ni kwa waathiriwa na jamaa zao.

No comments:

Post a Comment