Saturday, December 16, 2017

ZARIF: IRAN ITAISTAKI MAREMAKNI UMOJA WA MATAIFA

Zarif: Iran itaishtaki Marekani Umoja wa Mataifa
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu itayawasilisha Umoja wa Mataifa madai ya Nikki Haley, balozi wa Marekani katika umoja huo kwamba eti Iran imeipatia silaha harakati ya Ansarullah ya Yemen.
Katika ujumbe wa baruapepe aliotuma kwa shirika la habari la Russia la Sputnik, Dakta Zarif ameandika: Jamhuri ya Kiislamu itawasilisha malalamiko Umoja wa Mataifa dhidi ya madai yaliyotolewa na Marekani.
Siku ya Alkhamisi iliyopita, huku akiwa amesimama kando ya mabaki kadhaa ya vyuma, Haley alianzisha propaganda mpya dhidi ya Iran kwa kudai kwamba vyuma hivyo ni mabaki ya makombora ya Iran.
Pasi na kuashiria misaada ya silaha inayotolewa na Marekani kwa Saudi Arabia, silaha ambazo zinatumika kuwashambulia raia madhulumu wa Yemen, Haley aliituhumu Iran kuwa eti inaizatiti kwa silaha harakati ya Ansarullah ya Yemen kwa ajili ya kuishambulia kwa makombora Saudia.
Nikki Haley akiwa amesimama kando ya vyuma alivyodai kuwa ni mabaki ya makombora ya Iran
Naibu msemaji wa Umoja wa Mataifa Farhan Haq ameyakanusha madai hayo yaliyotolewa na balozi wa Marekani katika umoja huo.
Kwa msaada na uungaji mkono wa Marekani, tangu mwezi Machi mwaka 2015 Saudi Arabia imeanzisha uvamizi wa kijeshi dhidi ya Yemen na kuiwekea nchi hiyo mzingiro wa ardhini, baharini na angani. Moto wa vita uliowashwa na Saudia na waitifaki wake hadi sasa umesababisha makumi ya maelfu ya watu kuuawa na kujeruhiwa na mamilioni ya wengine kubaki bila makaazi.
Muungano huo vamizi wa kijeshi unaoongozwa na utawala wa Aal Saud umekuwa kila mara ukidai kwamba Iran inavipatia vikosi vya wananchi wa Yemen silaha na makombora na kwamba eti kwa kufanya hivyo inakwamisha utatuzi wa mgogoro wa nchi hiyo.
Hata hivyo viongozi wa Yemen wamesisitiza mara kadhaa kuwa uwezo wa kiulinzi na wa kujihami wa jeshi la nchi hiyo unatokana na nguvu zake za ndani na kwamba licha ya mzingiro wa kila upande uliowekwa na utawala wa Aal Saud, uwezo huo unaongezeka siku baada ya siku.
Utawala wa Aal Saud na Marekani hadi sasa zimeshindwa kufikia malengo yao nchini Yemen ya kuwaweka vibaraka wao madarakani kutokana na muqawama wa wananchi wa nchi hiyo.../

No comments:

Post a Comment