Monday, December 11, 2017

WANANCHI WA MAURITANIA WAANDAMANA KUMLAANI DONALD TRUMP

Wananchi wa Mauritania waandamana kumlaani Donald Trump
Wananchi wa Mauritania wameungana na Waislamu na wapenda haki katika kona zote za dunia kuendeleza maandamano ya kumlaani rais wa Marekani, Donald Trump kwa hatua yake ya kuitambua Quds kuwa mji mkuu wa utawala pandikizi wa Israel.
Mtandao wa gazeti la al Quds al Arabi umetangaza habari hiyo na kuongeza kuwa, maeneo mbalimbali ya Mauritania yameendelea kushuhudia maandamano ya kupinga uamuzi wa Trump kuhusiana na mji mtakatifu wa Baytul Muqaddas huku maelfu ya watu walioshiriki kwenye maandamano hayo wakitoa nara za "Mauti kwa Marekani," "Quds ni Yetu," "Mtake Msitake, Quds ni Mji Mkuu wa Palestina" na "Hatutoruhusu Kuporwa Quds." 
Wananchi na viongozi muhimu wa Mauritania katika maandamano

Watu wa matabaka mbalimbali nchini Mauritania wametoa matamko wakiitaka serikali ya nchi hiyo na nchi nyingine za Kiarabu na Kiislamu kukata uhusiano wao na Marekani kama njia ya kupinga uamuzi wa Donald Trump wa kuitambua rasmi Baytul Muqaddas kuwa kuwa eti ni mji mkuu wa Israel.
Donald Trump alitumia hotuba yake ya siku ya Jumatano kufanya uchokozi wa wazi kwa kuitangaza Quds ambayo ina Kibla cha Kwanza cha Waislamu kuwa eti ni mji mkuu wa utawala wa Kizayuni na hapo hapo akatoa amri ya kuanza mchakato wa kuhamishiwa Baytul Muqaddas, ubalozi wa Marekani ulioko Tel Aviv, mji mkuu wa utawala wa Kizayuni.
Viongozi wa nchi mbalimbali duniani nao wamelaani hatua hiyo wakiwemo wa Ulaya kama Uingereza na Papa Francis, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani. Hata Kim Jong-un, Kiongozi wa Korea Kaskazini ameubeza uamuzi huo wa rais wa Marekani wa kuitangaza Quds kuwa mji mkuu wa Israel na kusema kuwa, hakuna nchi inayoitwa Israel hata Baitul Muqaddas uwe mji mkuu wake.

No comments:

Post a Comment