Monday, December 25, 2017

JAMUHURI YA AL WIFAQ YALAANI HUKUMU YA KUNYONGWA ILIYOTOLEWA NA MAHAKAMA KUU YA KIJESHI YA BAHRAIN

Jumuiya ya al Wifaq yalaani hukumu ya kunyongwa iliyotolewa na mahakama kuu ya kijeshi ya Bahrain
Jumuiya ya Kiislamu ya al Wifaq ya Bahrain imelaani hukumu iliyotolewa na mahakama ya kijeshi ya nchi hiyo kwa raia wa nchi hiyo na kuitaja kuwa ni batili.
Jumuiya hiyo imesisitiza leo ikijibu hatua ya mahakama kuu ya kijeshi ya Bahrain ya kuwakatia hukumu ya kifo raia wa nchi hiyo kwamba kutishiwa kuuawa, kulazimishwa kukiri chini ya mateso kama kuadhibiwa kwa kushtushwa na umeme, kutishia kuwabaka ndugu na familia, kutekwa na kutiwa mbaroni kwa kificho kuwa ni vitendo visivyo vya kibinadamu wanavyofanyiwa raia wa Bahrain. 
Taaarifa ya Jumuiya ya Kiislamu ya al Wifaq imeongeza kuwa jamii ya kimataifa inapasa kuvunja kimya chake na kujiondoa katika kifungo cha wenzo wa mashinikizo wa mafuta na dola, na badala yake ionyeshe msimamo na ichukue hatua mkabala na maafa na jinai hizo zinazojiri huko Bahrain chini ya kivuli cha kukosekana uadilifu. 
Vikosi eti vya usalama vya Bahrain vikitawanya maandamano ya wananchi kwa gesi ya kutoa machozi  
Jumuiya ya al Wifaq imesisitiza kuwa fikra za ulipizaji kisasi haziwezi kudhibiti irada ya wananchi na kwamba vyombo vya mahakama vinawanyima wananchi wa Bahrain haki zao za msingi huku mahakama za kijeshi na vyombo vya usalama vikigeuzwa na kutumiwa kama wenzo na utawala ulioko madarakani katika kuwatesa raia wanaopinga utawala wa kidikteta na wa kifisadi wa nchi hiyo. Mahakama ya kijeshi ya Bahrain leo Jumatatu imewahukumu kunyongwa raia sita wengine wa nchi hiyo kwa tuhuma zisizo na msingi kwamba walihusika katika kupanga njama ya kumuuwa Sheikh Khalifa bin Ahmed Al Khalifah kamanda mkuu wa jeshi la nchi hiyo na vitendo vingine vya kigaidi. 

No comments:

Post a Comment