Wednesday, December 20, 2017

DRC: MKUTANO KATI YA RAIS KABILA NA MAGAVANA WAMALIZIKA GOMA

media
Rais wa DRC Joseph Kabila
Rais JOSEPH KABILA pamoja na viongozi wa ngazi za juu nchini DRC, waliokutana jijini GOMA tangu jumatatu wamehitimisha mkutano wao usiku wa kuamkia leo huku wakiwataka raia wa nchi hiyo kutojihusisha wala kujiunga na makundi ya waasi yanayotatiza usalama kwenye eneo la mashariki mwa nchi hiyo.
"Tumewaalika raia wa Congo kuilinda nchi yao piya twa shukuru wana jeshi ambao hivi sasa wajitahidi katika ulinzi wa raïa wilayani KASAI."
Huko magaavana walio shiriki mkutano huo walijulisha umuhimu wa mazungumzo yao dhidi ya raïa wa Congo DRC, kama alivyo julisha LOLA KISANGA liwali wa Jimbo la UELE.
"Twatazama yote tukiona jinsi gani usalama wa kweli waweza rejea na kusaidia kwa ujenzi bora wa nchi yetu"
Raia wamepokeaje yaliyo zungumziwa jijini Goma na viongozi serikali ya Congo DRC !
"Ikiwa hakuna upendo haya yote ni kupoteza mda.cha maana magavana hao watimize waliyo zungumza."
Licha ya kutozungumza na wanahabari kwenye mkutano huo, duru za ndani zinaeleza kuwa rais Joseph Kabila aliwakosoa viongozi ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya rushwa na ubadhirifu wakati huu wakijua anaelekea kumaliza muda wake.
Viongozi hao wa serikali ya Congo DRC wamethibitisha kuendesha mkutano kama na huo jijini MBANDAKA mwezi machi mwaka ujao kwa lengo la kuboresha zaidi uchumi na maendeleo ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

No comments:

Post a Comment