Wednesday, December 20, 2017

UN YALAANI KITENDO CHA ISRAEL KUMPIGA RISASI KUMUUA MPALESTINA MLEMAVU

UN yalaani kitendo cha Israel kumpiga risasi na kumuua Mpalestina mlemavu
Kamishna Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa amesema amestaajabishwa sana na kitendo cha jeshi la Israel kumuua kwa kumpiga risasi mtu mwenye ulemavu aliyekuwa anaelekea msikitini siku ya Ijumaa.
Zeid Ra'ad Al Hussein  Kamishna Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa ametoa kauli hiyo kufuatia ripoti kwamba mtu huyo Ibrahim Abu Thurayeh aliuawa shahidi akiwa kwenye kitimwendo chake.
Ibrahim alikuwa miongoni mwa mamia ya Wapalestina walioandamana Ijumaa karibu na uzio kati ya Ukanda wa Gaza na Israel, wakipinga hatua ya Marekani kutambua mji wa Quds (Jerusalem) kuwa eti ni mji mkuu wa utawala bandia wa Israel.
Zeid amesema taarifa zinadhihirisha kuwa jeshi la Israel lilitumia nguvu nyingi kupita kiasi kitendo ambacho ni kinyume na sheria za kimataifa za kibinadamu.
Shahidi Ibrahim Abu Thureya
Hili ni janga la pili kumkuta Ibrahim ambapo mwaka 2008 makombora yaliyorushwa na Israel yalimkataa miguu yake miwili.
Afisa huyo wa Umoja wa Maaifa ametaka hatua za kisheria zichuliwe dhidi ya waliotekeza jinai hiyo.

No comments:

Post a Comment