Tuesday, December 26, 2017

RAILA ODINGA : NITAAPISHWA MAPEMA MWAKA 2018 KAMA RAIS WA WATU

media
Kiongozi wa Muungano wa Upinzani Kenya, Raila Odinga.
Kiongozi wa muungano wa upinzani nchini Kenya NASA, Raila Odinga amesema ataapishwa kama rais wa watu mapema mwaka 2018.
Katika ujumbe wake wa Krismasi, Odinga ameonya kuwa Kenya inaelekea kuwa taifa la Kidikteta na kuwataka wafuasi wake kuendelea kuunga mkono mikakati ya upinzani.
Serikali imeonya kuwa Odinga atafunguliwa mashtaka ya uhaini iwapo ataapishwa, onyo ambalo kiongozi huyo wa NASA amesema yuko tayari kukabiliana nalo  ikiwa ndio itakuwa njia ya kuleta haki ya kisiasa katika taifa hilo.
Iwapo Odinga, atatekeleza mipango yake, itaendeleza kuzua mvutano wa kisiasa katika taifa hilo ambalo limemaliza Uchaguzi hivi karibuni.
Marekani imetaka kuwepo kwa mazungumzo kati ya Odinga na Kenyatta, na kumhimiza kiongozi huyo wa NASA kutojiapisha kwa kile inachosema kitendo hicho kitaendelea kuzua mzozo wa kisiasa.
Kenyatta amenukuliwa mara kadhaa akisema kuwa, yuko tayari kuzungumza na Odinga lakini mazungumzo hayo yawe ni kuhusu maendeleo ya nchi huku Odinga akisema atashiriki tu kuhusu mazungumzo yatakayokuwa na ajenda ya namna ya kuwa na Uchaguzi wa urais utakaokuwa huru na haki.
Chanzo:RFI

No comments:

Post a Comment