Monday, December 11, 2017

WANAWAKE WALIONYANYASWA KINGONO NA TRUMP WAITAKA KONGRESI KUFANYA UCHUNGUZI

Wanawake walionyanyaswa kingono na Trump waitaka Kongresi kufanya uchunguzi
Wanawake wanaomtuhumu Rais Donald Trump wa Marekani kwamba aliwanyanyasa kingono wamelitaka Bunge la nchi hiyo (Kongresi) kufanya uchunguzi kuhusu kashfa za kimaadili za kiongozi huyo.
Wanawake hao wanaosema walinyanyaswa kijinsia na Trump walitarajiwa kukutana leo kwa mara ya kwanza na kutoa wito wa kuanza uchunguzi kuhusu kashfa za kingono za Donald Trump.
Wakati huo huo balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Nikki Haley amesema kuwa wanawake wanaomtuhumu Rais Donald Trump kuwa aliwanyanyasa kijinsia wanapaswa kuzikilizwa.
Haley amesema wanawake hao wanapaswa kusikilizwa na kesi yao inapaswa kushughulikiwa.
Gavana huyo wa zamani na mmoja kati ya wanawake wenye vyeo vya juu katika utawala wa Trump, amesema wakati umefika wa kutafakari kwa kina kuhusu jinsi wanawake wanavyotendewa nchini Marekani.
Nikki Haley
Matamshi hayo ya balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa yanakwenda kinyume kabisa na sisitizo la serikali ya nchi hiyo ambayo imekuwa ikidai kuwa kashfa za kuwanyanyasa kijinsia wanawake zinazomkabili Donald Trump hazina msingi.
Makumi ya wanawake wamemtuhumu Rais Donald Trump wa Marekani kuwa aliwanyanyasa kingono ikiwa ni pamoja na kuwapapasa papasa, kuwabusu kwa kuwalazimisha na kutumia maneno machafu na ya utovu wa maadili.

No comments:

Post a Comment