Monday, December 25, 2017

WATU WASIOPUNGUA 15 WAUAWA KATIKA MASHAMBULIZI YA ANGA YA SAUDI HUKO SANA'A NA KATIKA MIJI MINGINE

Watu wasiopungua 15 wauawa katika mashambulizi ya anga ya Saudi huko Sana'a na katika miji mingine
Televisheni ya al Masirah imetangaza kuwa watu wasiopungua 15 wameuawa katika mashambulizi mapya ya anga ya Saudi Arabia katika maeneo mbalimbali huko Yemen, ukiwemo mji mkuu Sana'a.
Ndege za kivita za Saudi Arabia mapema leo zimeyashambulia mashamba mawili katika wilaya ya Zabid katika mkoa wa Hudaydah na kuua watu wanane wakiwemo wanawake wawili. Wanawake wengine wawili wamejeruhiwa pia katika mashambulizi hayo.
Makazi ya raia katika mkoa wa Hudayadah yaliyoshambuliwa na ndege za kivita za Saudia 
Ndege hizo za kivita za Saudia leo pia zilifanya mashambulizi kadhaa katika mji mkuu wa Yemen Sana'a na kuua raia saba na kujeruhi wengine watano. Watoto watatu na wanawake wawili ni miongoni mwa raia waliojeruhiwa huko Sana'a huku watu wengine wawili wakiwa hawajulikani walipo. Televisheni ya al Masirah imeripoti kuwa nyumba moja iliyolengwa na ndege za kivita za Saudi Arabia katika mji mkuu Sana'a imeharibiwa kikamilifu na kwamba wafanyakazi wa huduma za uokoaji waliokuwa wakiwatafuta majeruhi waliofunikwa na vifusi vya nyumba hiyo nao pia wamelengwa na ndege hizo za kivita za Saudia. Watu walioshuhudia wamesema kuwa idadi ya watu waliouawa kwenye mashambulizi hayo ya Saudia huenda ikaongezeka. 

No comments:

Post a Comment