Wednesday, December 20, 2017

UGANDA NA DRC KUSHIRIKIANA KATIKA KUPAMBANA NA WAASI WA ADF

Uganda na DRC kushirikiana katika kupambana na waasi wa ADF
Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimekubaliana kuimarisha utaratibu wa mawasiliano na kupeana taarifa za kiintelijensia kwa ajili ya kupambana na waasi wa ADF kufuatia mashambulizi yao dhidi ya vikosi vya walinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa.
Msemaji wa jeshi la Uganda Brigedia Richard Karemire amesema serikali ya Uganda na maofisa wa Kivu ya Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekuwa na mkutano wa usalama.
Msemaji huyo amesema kupeana taarifa kutasaidia vikosi vijiandae kuwazuia waasi kujipenyeza ndani na mashambulizi yanayoweza kufanywa na ADF.
Hivi karibuni askari 14 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)  waliuawa , 44 walijeruhiwa na wengine wawili  hawajulikani walipo kufuatia hujuma ya waasi wa ADF.
Askari wa Tanzania walio katika kikosi cha kulinda amani cha UN nchini DRC
Tukio hilo lilitokea Desemba 7,2017 katika kambi ndogo iliyopo katika daraja la Mto Simulike, kaskazini mashariki mwa Wilaya ya Beni, Jimbo la Kivu.
Askari waliouawa walikuwa ni sehemu ya askari 3,000 wa tume ya kulinda amani ya umoja wa mataifa MONUSCO yenye askari kutoka Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment