Monday, December 25, 2017

BUNGE LAIRAN LAPITISHA: QUDS NI MJI MKUU WA KUDUMU WA PALESTINA

Bunge la Iran lapitisha: Quds ni mji mkuu wa kudumu wa Palestina
Wabunge wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran leo wamepitisha mpango wa dharura wa kuunga mkono Mapinduzi ya Kiislamu ya watu wa Palestina na kusisitiza kwamba Baitul Muqaddas utakuwa mji mkuu wa kudumu wa nchi ya Palestina.
Mpango huo wa dharura umepitishwa kwa kura 187 za ndiyo, 15 za hapana huku wabunge tisa kati ya wabunge wote 233 waliohudhuria kikao hicho cha wazi cha bunge la Iran wakiamua kutopiga kura.
Mpango huo uliopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unaunganishwa kwenye Ibara nambari moja ya sheria ya kuunga mkono Mapinduzi ya Kiislamu ya watu wa Palestina.
Mpango huo utawasilishwa kwenye kamati husika ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu na kuwekwa kwenye ajenda za kujadiliwa na kupitishwa rasmi na bunge hilo ndani ya muda wa masaa 48 yajayo.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni muungaji mkono thabiti wa mapambano ya Wapalestina na imekuwa ikitoa wito kwa Waislamu wote duniani kuungana dhidi ya utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel ambao Tehran haiutambui asilani kuwa ni moja ya nchi za ulimwengu.
Rais Hassan Rouhani akishiriki kwenye maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds kuunga mkono ukombozi wa Palestina
Itakumbukwa kuwa tarehe 6 Desemba, Rais Donald Trump wa Marekani aliamsha hasira za walimwengu kwa kutangaza kuitambua Baitul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala haramu wa Israel na kuagiza zichukuliwe hatua za maandalizi ya kuuhamishia katika mji huo ubalozi wa Marekani ulioko Tel Aviv.
Hata hivyo siku ya Alkhamisi iliyopita, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio kwa wingi mkubwa wa kura 128 za 'ndiyo' dhidi ya 9 tu za 'la' kupinga tangazo hilo la rais wa Marekani na kumtaka abadilishe uamuzi wake huo. 
Kwa mujibu wa azimio hilo, Umoja wa Mataifa hautoitambua Quds kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel.../

No comments:

Post a Comment