Tuesday, December 26, 2017

NJAMA ZA SERIKALI YA NIGERIA DHIDI YA SHEIKH IBRAHIMU ZAKZAKY

Njama za serikali ya Nigeria dhidi ya Sheikh Ibrahim Zakzaky
Mjumbe wa ngazi ya juu wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria amesema kuwa, serikali ya nchi hiyo inatekeleza njama za kumuua shahidi Sheikh Ibrahim Zakzaky kiongozi wa harakati hiyo.
Ibrahim Suleiman ameashiria pingamizi la kila mara la serikali ya Nigeria kuhusiana na takwa la familia ya Sheikh Zakzaky la kumpeleka nje ya nchi kiongozi huyo wa Kiislamu kwa ajili ya matibabu licha ya hali ya mwanazuoni huyo kuwa mbaya. Mwakilishi huyo wa ngazi ya juu wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria ameongeza kuwa upo uwezekano kuwa njama zinafanywa ili kumuua shahidi pole pole Sheikh Zakzaky. Sheikh Ibrahim Zakzaky Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria na mkewe walitiwa mbaroni katika shambulizi lililofanywa Disemba 13 mwaka juzi na wanajeshi wa Nigeria katika Husseiniya iliyopo katika mji wa Zaria jimboni Kaduna kaskazini mwa nchi hiyo. Mamia ya waumini wa Kiislamu wakiwemo watoto watatu wa Sheikh Zakzaky waliuliwa shahidi katika tukio hilo.
Hassan al-Banna, mjumbe wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria sambamba na kuashiria mashtaka ya harakati hiyo dhidi ya serikali ya Nigeria katika Umoja wa Afrika amesema kuwa, licha ya kutolewa amri ya mahakama ya kuachiliwa huru Sheikh Zakzaky pamoja na mkewe, lakini serikali ya Abuja imekataa katakata kutekeleza amri hiyo. Kwa muda sasa serikali imekuwa ikitekeleza siasa za chuki na adawa dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.
Maandamano ya kutaka kuachiliwa huru Sheikh Ibrahim Zakzaky
Kutiwa mbaroni Sheikh Ibrahim Zakzaky na kushadidi mashinikizo dhidi ya Waislamu sambamba na kupigwa marufuku mkusanyiko wa aina yoyote ile wa Waislamu wa nchi hiyo ni miongoni mwa siasa ambazo zimekuwa zikitekelezwa na serikali ya Rais Muhammadu Buhari dhidi ya Waislamu wa Nigeria. 
Hatua hizo zinatekelezwa katika hali ambayo, hivi karibuni Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International sambamba na kutahadharisha kuhusiana na kutoweka idadi kadhaa ya Waislamu wa Nigeria, lilikosoa vikali utendaji wa serikali ya Abuja katika uwanja huo na kuitaka serikali hiyo ianzishe uchunguzi kuhusiana na kutoweka wanachama 600 wa Harakati hiyo ya Kishia.
Wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, serikali ya Nigeria inachukua hatua hizo chini ya ushawishi wa siasa za utawala wa Saudia, Marekani na utawala dhalimu wa Israel. Ni kwa muda sasa ambapo Wazayuni baada ya siasa zao kugonga mwamba katika eneo la Mashariki ya Kati na kutengwa, sasa wameligeukia bara la Afrika na wamo mbioni kutafuta washirika wao wapya katika bara hilo. 
Sheikh Ibrahim Zakzaky, Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria
Katika fremu hiyo, hivi karibuni baadhi ya makamanda wa jeshi la Nigeria  walikutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa kijeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel. Saudia ni nchi nyingine ambayo imekuwa ikihaha kuhakikisha kuwa inakuwa na satuwa na ushawishi barani Afrika. 
Misaada ya siri na dhahiri ya kifedha na kijeshi ya Saudia kwa nchi za bara hilo na mkabala wake nchi hizo zisalimu amri mbele ya matakwa ya utawala wa Riyadh ni baadhi ya mikakati inayofanywa na watawala wa Aal Saud. Marekani nayo kwa kuiuzia silaha na zana za kijeshi serikali ya Nigeria imekuwa ikisaidia katika kukandamizwa Waislamu wa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika. Katika uga huo, hivi karibuni Abdul-Rahman Abubakar Mkuu wa Kamati ya Kufuatilia Kuachiliwa Huru Sheikh Ibrahim Zakzaky, sanjari na kuitumia barua serikali ya Marekani na kuashiria rekodi ambayo haijawahi kushuhudiwa ya serikali ya Nigeria kukiuka na kukandamiza haki za binadamu, ameitaka Washington iache kuiuzia silaha nchi hiyo.
Filihali kwa kuzingatia uadui wa tawala tatu za Israel, Saudia na Marekani dhidi ya harakati za kupigania uhuru za Kiislamu na ushawishi wa tawala hizo nchini Nigeria, suala la hatari ya kuuawa shahidi Sheikh Ibrahim Zakzaky na setikali ya Nigeria kufanya hilo kwa makusudi ni jambo ambalo linazidi kupata nguvu

No comments:

Post a Comment