Monday, December 25, 2017

CHINA YAZINDUA NDEGE KUBWA INAYOWEZ KUTUA NCHI KAVU NA MAJINI

China yazindua ndege kubwa zaidi inayoweza kutua nchi kavu na majini
China imezindua ndege ya "Jiaolong" AG600 ambayo ni ndege kubwa zaidi duniani inayoweza kutua nchi kavu na majini.
Ndege hiyo imeundwa kikamilifu nchini China na jana ilifanikiwa kuruka kwa majaribio. Ndege hiyo ni kwa ajili ya kukabiliana na ajali za moto misituni, na uokoaji watu majini. Inaweza kuvuta maji tani 20 ndani ya sekunde 20, na kuzima moto katika eneo la mita za mraba zaidi ya 4,000 mara moja, huku ikiweza kuwaokoa watu 50 baharini mara moja. Mbali na kuzima moto na kuwaokoa watu, pia inaweza kutumiwa katika uchunguzi na uhifadhi wa mazingira baharini.
Meli ya kivita ya China yenye uwezo wa kusheheni ndege
Ndege hiyo pia inaweza kutumika kijeshi na inatathminiwa kuwa uzinduzi wake ni katika jitiahda za China za kuimarisha uwezo wake wa kiulinzi.
Mapema mwaka huu, China ilizindua meli yake ya kwanza ya kivita yenye kusheheni ndege (aircraft carrier) iliyoundwa nchini humo.

No comments:

Post a Comment