Friday, September 1, 2017

TUME YA UCHAGUZI DRC KUTANGAZA RATIBA YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Corneille Nangaa amesema ratiba ya Uchaguzi mkuu itatangazwa hivi karibuni.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya tume hiyo kutangaza kuwa jumla ya wapiga kura milioni 40 wameandikishwa kwenye majimbo 24 na kwamba kuanzia tarehe nne itaanza kuandikisha wapiga kura kwenye majimbo mawili ya Kasai.
Serikali ya Kinshasa imesema zoezi la kuandikisha wapiga kura litaanza kukamilika kabla ya kutangazwa mambo mengine.
Mapema wiki hii Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya DRC (CENI) ilisema, zoezi la kuhakiki na kuandikisha wapiga kura wapya kwenye majimbo mawili ya Kasai ambako kumeshuhudiwa machafuko hivi karibuni, litaanza September 4 na kisha kuendelea kwenye majimbo mengine 24
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi CENI, Corneille Nangaa amewataka wananchi kuwasaidia maofisa wake kufanya kazi ya kuandaa uchaguzi kwa uhuru.
Rais Joseph Kabila
Katika hatua nyingine upinzani umekosoa takwimu za hivi karibuni zilitolewa na tume hiyo ukisema kwamba kiwango kikubwa hakiko sawa.
CENI ilisema jumla ya wapiga kura milioni 40 wameandikishwa kwenye majimbo mengine 24 huku taifa hilo likiwa na jumla ya raia milioni 70 wengi wao wakiwa bado hawajaandikishwa.
Mgogoro wa ndani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo uliibuka baada ya kuahirishwa tarehe ya uchaguzi wa rais na kadhalika sisitizo la Rais Joseph Kabila la kutaka kuendelea kubakia madarakani. Licha ya kutiwa saini makubaliano baina ya wapinzani na serikali juu ya kufanyika uchaguzi wa rais tarehe 31 mwezi Disemba mwaka huu, lakini inaonekana kuwa, uchaguzi huo hautaweza kufanyika katika tarehe iliyopangwa.

No comments:

Post a Comment