Friday, September 22, 2017

MWANASHERIA MKUU: KENYA HAIKO KWENYE HATARI YA MGOGORO WA KIKATIBA

Mwanasheria Mkuu: Kenya haiko kwenye hatari ya mgogoro wa kikatiba
Mwanasheria Mkuu wa Kenya amesema kuwa nchi hiyo haitakabiliwa na mgogoro wa kikatiba au wa kisiasa hata kama uchaguzi rais wa marudio uliopangwa kufanyika Oktoba 26, umesogezwa tarehe hadi baada ya mwishoni mwa Oktoba.
Githu Muigai ameongeza kuwa, serikali ya sasa itaendelea kuwepo madarakani kihalali kwa nguvu kamili ya kikatiba hadi uchaguzi mpya utakapokamilika na kiongozi mpya kuapishwa.
Mahakama ya Juu ya Kenya mwezi huu ilitengua ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa Agosti 8 ikiashiria kuwepo kasoro na kuiamuru Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka kuandaa uchaguzi mpya hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Oktoba. Uhuru Kenyatta atachuana kwa mara nyingine na hasimu wake kutoka muungano wa Nasa, Raila Odinga.
Mwanasheria Mkuu wa Kenya alikuwa akijibu matamshi ya wakili wa Odinga katika shauri lililopelekea kutenguliwa ushindi wa Kenyatta, Bwana James Orengo aliyesema kuwa muhula wa urais wa Kenyatta utafikia kikomo iwapo uchaguzi huo wa marudio hautafanyika hadi kufikia mwishoni mwa Oktoba na hivyo kuitumbukiza nchi katika mgogoro wa kikatiba.
Wakili James Orengo ambaye amepingana na kauli ya Mwanasheria Mkuu wa Kenya 
Naye kiongozi wa  muungano wa NASA nchini Kenya Raila Odinga amesema anaamini kuwa, muhula wa kuwa madarakani Uhuru Kenyatta utamalizika katika kipindi cha siku 60 baada ya Mahakama ya Kilele kutoa uamuzi wa kutengua matokeo ya uchaguzi wa rais tarehe Mosi Septemba. Odinga amesema hatashiriki uchaguzi iwapo baadhi ya masharti hayatatimizwa likiwemo la kutaka kuondolewa baadhi ya maafisa wa Tume Huru ya Uchaguzi

No comments:

Post a Comment