Saturday, September 16, 2017

HUFFINGTON POST: WAMAREKANI NI WABAGUZI

Matokeo ya uchunguzi wa taasisi mbili za kisayansi za Marekani yanaeleza kuwa, watu wengi wa nchi hiyo wana mielekeo ya kibaguzi licha ya kutoa madai ya kupinga fikra ya kuwatambua wazungu kuwa ndio wanadamu walio juu na bora kuliko wengine.
Gazeti la Huffington Post linalochapishwa nchini Marekani limeripoti kuwa, matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa kwa pamoja na taasisi ya Ipswich na Chuo Kikuu cha Virginia yameonesha kuwa, ingawa idadi ya waungaji mkono wa manazi mamboleo na fikra kwamba wazungu wako juu na ni bora zaidi kuliko wanadamu wengine, lakini baadhi ya fikra na mitazamo ya kibaguzi na ya kufurutu mipaka inaungwa mkono kwa wingi nchini humo. 
Uchunguzi huo wa maoni ulifanyika kuanzia tarehe 21 Agosti hadi tarehe 5 Septemba, yaani wiki kadhaa tu baada ya mapigano ya wabaguzi wa rangi katika jimbo la Virginia.
Maandamano ya kupinga ubaguzi nchini Marekani
Matokeo ya uchunguzi huo pia yameonesha kuwa, asilimia 8 ya washiriki wamesema kuwa, wanaiunga mkono harakati ya kitaifa ya wazaungu wabaguzi na kwamba asilimia 39 kati yao wanaamini kuwa, wazungu wanashambuliwa nchini Marekani!
Uchunguzi huo umebaini kuwa, mtu mmoja kati ya kila Wamarekani sita anaamini kwamba, ndoa zinapaswa kufanyika baina ya watu wa mbari moja na si kwa mfano kati ya Wamarekani weusi na wazungu.  
Kyle Kondick Mkurugenzi wa Mahusiano ya Kisiasa wa Chuo Kikuu cha Virginia anasema matokeo ya uchunguzi huo yanaonesha kuwa, jamii ya Marekani ina mitazamo inayokubali ubaguzi wa rangi.    

No comments:

Post a Comment