Friday, September 22, 2017

SERIKALI NIGERIA YAELEZA WASIWASI WAKE KUHUSU SILAHA ZA MAGENDO NCHINI HUMO

Serikali Nigeria yaeleza wasiwasi wake kuhusu silaha za magendo nchini humo
Serikali ya Nigerfia imetangaza kwamba, ina wasiwasi kuhusu silaha zinazoingizwa kwa wingi nchini humo kupitia njia za magendo.
Msemaji wa Idara ya Forodha ya Nigeria, Joseph Attah amesema kuwa matokeo ya awali ya uchunguzi uliofanyika katika uwanja huo yanaonesha kuwa, wahusika wa magendo ya silaha nchini Nigeria ni makundi ya mafia yaliyoko nchini Uturuki.
Attah ameongeza kuwa, tangu mwanzoni mwa mwaka huu silaha zaidi ya elfu tatu zimegunduliwa na kukamatwa katika bandari ya Lagos kutoka Uturuki. 
Hadi sasa ubalozi wa Uturuki nchini Nigeria haujasema lolote kuhusu tuhuma hizo za magendo ya silaha kutoka Uturuki kelekea Nigeria. 
Silaha za magendo zinaingizwa Nigeria kutoka Uturuki
Maafisa wa Idara ya Forodha ya Nigeria wanatazamiwa kufanya mazungumzo na wenzao wa serikali ya Uturuki akiwemo balozi wa nchi hiyo mjini Abuja kuhusu maudhui ya magendo ya silaha zinazoingizwa nchini humo kutoka Uturuki. 
Nigeria imekuwa ikisumbuliwa na machafuko makubwa hususan katika maeneo ya kaskasini mwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment