Friday, September 22, 2017

KAMAND WA JESHI LA ISRAEL: NI VIZURI ISRAEL IENDELEE KUJIEPUSHA KUINGIA VITANI NA HIZBULLAH

Kamanda wa jeshi la Israel: Ni vizuri Israel iendelee kujiepusha kuingia vitani na Hizbullah
Mkuu wa Majeshi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel amesema kuwa, ni kwa maslahi ya utawala huo ikiwa utaendelea kujitenga mbali na vita vyovyote na Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya nchini Lebanon.
Gadi Eizenkot, aliyasema hayo jana Alkhamisi katika mahojiano na mtandao wa habari wa Kizayuni wa Walla na gazeti la utawala huo la Yedioth Ahronoth na kuongeza kuwa, harakati ya Hizbullah ndio adui mkubwa na hatari anayeitia wasi wasi mkubwa Israel, hasa kwa kuzingatia kuwa ina uwezo mkubwa wa kijeshi huku ikiwa na ngome kadhaa za kijeshi Lebanon na Syria kiasi cha kuifanya iwe jeshi kubwa.
Askari wa Israel wakilia mithili ya watoto baada ya kushindwa katika vita vya mwaka 2006 na Hizbullah
Amesisitiza kuwa, harakati hiyo ya muqawama imekuwa ikipambana nchini Syria kwa miaka kadhaa sasa huku ikiwa na vikosi kamili vya kivita sambamba na kutoa misaada ya kijeshi na intelejensia za kivita kwa jeshi la Syria. Ameongeza kuwa, hata kama jeshi la Israel lina nguvu, lakini linatakiwa liendelee kujizuia kuanzisha vita vyovyote na harakati hiyo ya Kiislamu. Mkuu wa Majeshi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel sambamba na kujaribu kuwapa utulivu Wazayuni kwamba hivi sasa  eti ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu ( Israel) kuna usalama na kwamba, jeshi la Israel limejiandaa kukabiliana na aina yoyote ya changamoto na tishio dhidi yake, amesema kuwa, ni lazima utengamano uliopo kwa sasa uendelee kuwepo badala ya kuingia vitani na Hizbullah.
Wanamapambano wa muqawama wa Hizbullah
Itakumbukwa kuwa katika vita vya siku 33 vya mwaka 2006 kati ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na harakati ya muqawama ya Hizbullah, Israel ilipata hasara kubwa na kulazimika kurudi nyuma. Katika sehemu nyingine Gadi Eizenkot amesema kuwa uwepo wa serikali ya mamlaka ya ndani ya Palestina inaoongozwa na Mahmoud Abbas ni kwa maslahi ya utawala wa Kizayuni kwa kuwa kuna mahusiano mazuri ya kiusalama kati ya Israel na serikali hiyo.

No comments:

Post a Comment