Friday, September 22, 2017

HATIBU WA SWALA YA IJUMAA TEHRAN: TRUMP NI MTU MWENYE AKILI FINYU, KIDHABI NA MPENDA VITA

Hatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Trump ni mtu mwenye akili finyu, kidhabi na mpenda vita
Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema kuwa hotuba iliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ni ya kipumbavu na kwamba Trump ni mtu mwenye akili finyu, kidhambi na mpenda vita.
Katika hutuba yake ya hivi karibuni kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Rais huyo wa Marekani aliituhumu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambayo ni miongoni mwa mihimili na nguzo kuu za kupambana na magaidi katika eneo la Mashariki ya Kati, kuwa inaunga mkono ugaidi.
Katika hotuba zake za leo kwenye Swala ya Ijumaa, Hujjatul Islam Walmuslimin Kazem Seddiqi amesema matamshi yasiyo ya kidiplomasia ya Trump ni kielelezo cha hasira na kuchanganyikiwa. 
Donald Trump
Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran ameashiria kufeli kwa njama za Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati na kusema: Katika miezi ya hivi karibuni Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wapiganaji wa Hizbullah na Russia wametoa kipigo kikali kwa magaidi wanaoungwa mkono na kusaidiwa na Marekani na washirika wake. 
Hujjatul Islam Walmuslimin Seddiqi ameongeza kuwa, Daesh, al Qaida, Taliban na magenge mengine kadhaa ya kigaidi ni watoto wa Marekani na Saudi Arabia na kusisitiza kuwa: Nchi hizo mbili zimetumia mamilioni ya fedha za watu wao kwa ajili ya kuanzisha makundi kama hayo ya kigaidi. Amesema, Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ni mapinduzi ya watu waliodhulumiwa kote duniani na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu daima itaendelea kuwasaidia watu wa Iraq na Syria katika vita vyao dhidi ya magaidi. 
Magaidi wa Daesh wakiwamiminia risasi raia wa Iraq
Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran pia amewapa mkono wa pole Waislamu kote duniani kwa mnasaba wa kuwadia mwezi wa Muharram na kusisitzia kuwa, Imam Hussein bin Ali (as) aliuawa katika mwezi huu katika mapambano yake dhidi ya mfumo na utawala wa kidhalimu na kibeberu.   

No comments:

Post a Comment