Sunday, May 28, 2017

TRUMP AWAAMBIA WASHAURI MAREKANI KUJITOWA MKATABA WA PARIS

Mtandao wa habari wenye makao yake mjini Washington, Marekani umeripoti kwamba Rais Donald Trump amewaambia "watu anaowamini" ataachana na makubaliano ya kihistoria ya tabia nchi yaliofikiwa Paris Ufaransa.

China | Illegale Stahlfabriken unterlaufen Chinas Emissionsgesetze (Getty Images/K. Frayer)
Mtandao wa habari wenye makao yake mjini Washington nchini Marekani umeripoti kwamba Rais Donald Trump wa Marekani amewaambia "watu anaowamini" ataachana na makubaliano ya kihistoria ya tabia nchi yaliofikiwa Paris Ufaransa ambayo mtangulizi wake Barack Obama ameyasaini hapo mwaka 2016 kupunguza kiwango cha utowaji wa hewa ukaa gesi yenye kuchafuwa mazingira duniani.
Kutokuwepo kwa hali ya uhakika kuhusiana na msimamo wa Marekani juu ya suala la tabia nchi kumewatibuwa viongozi wenzake katika mkutano wa kilele wa nchi za G7 zenye maendeleo makubwa ya viwanda duniani ambao umemalizika Jumamosi huko Taormina, Sicily nchini Italia bila ya kuwepo kwa maafikiano ya sauti moja kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Rais Donald Trump amesema atotowa uamuzi wa mwisho wiki hii iwapo Marekani iendelee kubakia katika makubaliano ya tabia nchi yaliyofikiwa Paris au ijitowe. Trump ametowa tangazo hilo la ghafla katika mtandao wa Twitter baada ya kuhimili shinikizo kutoka kwa viongozi wa Ulaya waliokuwa wakimtaka abakie katika mkubaliano hayo.
Vyanzo vya kuaminika
G7 Gipfeltreffen Donald Trump spricht mit Angela Merkel und Beji Caid Essebsi (Reuters/J. Ernst)
Viongozi wa nchi za G7 katika mazungumzo.
Ikitaja vyanzo vitatu vyenye uwelewa wa moja kwa moja wa mipango ya Trump ukurasa wa kutowa habari wenye kuheshimika Axios umeripoti Jumamosi kwamba kiongozi huyo wa Marekani amewaambia washauri wake wakuu ataitowa Marekani kwenye makubaliano ya tabia nchi yaliofikiwa Paris mwaka 2015.
Ukurasa huo umeanzishwa mwaka jana na mmojawapo wa wasisi wenza wa kisiasa na mkuu wa zamani wa waandihishi  wa Ukulu ya White House.Ukurasa huo wa Axios umesema iwapo ni kweli utabiruwa sera za tabia nchi za mtangulizi wake Barack Obama na kutuma ishara ya mapambano kwa dunia nzima kwamba suala la kuongezeka kiwango cha joto duniani si miongoni mwa vipau mbele vya Trump.
Ukurasa huo wa mtandao umekiri kwamba rais huyo tajiri mkubwa kabisa amebadili mawazo yake juu ya ahadi kadhaa madhubuti alizotowa wakati wa kampeni tokea aingie madarakani hapo mwezi wa Januari.
Uamuzi wiki hii
G7 Gipfeltreffen in Taormina Italien US-Präsident Donald Trump (Reuters/D. Martinez)
Rais Donald Trump wa Marekani.
Trump amewaambia viongozi katika mkutano wa G7 kundi la mataifa lenye maendeleo makubwa ya viwanda duniani huko Italia hapo Jumamosi(27.05.2017) kwamba atatowa uamuzi wake kuhusu iwapo Marekani iendelee kuunga mkono makubaliano ya kihistoria ya tabia nchi katika kipindi kisichozidi wiki moja.Nchi za kundi la G7 zinajumuisha miongoni mwa nchi nyengine Ujerumani,Uingereza,Canada,Ufaransa na Japani.
"Nitatowa uamuzi wa mwisho juu ya mkataba wa Paris wiki ijayo!" ameandika Trump kwenye mtandao wa Twitter bada ya huko nyuma kuita ongezeko la joto duniani kuwa ni "dhihaka".
Ukosefu wa kujitolea wa Trump kwa makubaliano hayo ya tabia nhi ambayo yanazitaka nchi kujifunga kupunguza kiwango kikubwa sana cha utowaji wa hewa ukaa kupunguza madhara ya kuongezeka kiwango cha ujoto duniani kumewatibuwa washirika wa jadi wa Marekani ikiwemo Ujerumani.
Kansela Angela Merkel wa Ujerumani amesema mazungumzo ya G7 kuhusu tabia nchi yamekuwa na matatizo magumu sana.Amewaambia waandishi wa habari majadiliano kuhusu tabia nchi yalikuwa magumu sana na kama sio kusema hayaridhishi kabisa" na kwamba "hakuna dalili iwapo Marekani itabakia katika makubaliano ya Paris au hapana."
Mkubaliano hayo ya kihistoria ya tabia nchi yalisainiwa na nchi 195 mjini Paris hapo mwezi wa Disemba mwaka 2016 na kuanza kufanya kazi miezi 11 baadae.Mkataba huo umezifunga nchi kuzuwiya kuongezeka kwa ujoto kupindukia nyuzi joto mbili kiwango kilichokuweo kabla ya enzi za viwanda.

No comments:

Post a Comment